Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 10:4 - Swahili Revised Union Version

Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Uvivu husababisha umaskini, lakini mkono wa mtu wa bidii hutajirisha.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Uvivu husababisha umaskini, lakini mkono wa mtu wa bidii hutajirisha.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Uvivu husababisha umaskini, lakini mkono wa mtu wa bidii hutajirisha.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 10:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa siku ileile, watumwa wa Isaka wakaja wakampasha habari za kile kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, Tumeona maji.


Akusanyaye wakati wa joto ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.


Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.


Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.


Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.


Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.


Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharibifu.


Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.


Mtu mvivu hutia mkono wake katika sahani; Wala hataki hata kuupeleka kinywani pake.


Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.


Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.


Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.


Kwa sababu ya uvivu paa hunepa; Na kwa ulegevu wa mikono nyumba huvuja.


Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa mhuri na Baba, yaani, Mungu.


Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mnajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.