Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 11:24 - Swahili Revised Union Version

24 Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

24 Atoaye kwa ukarimu huzidi kutajirika; lakini bahili huzidi kudidimia katika umaskini.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

24 Atoaye kwa ukarimu huzidi kutajirika; lakini bahili huzidi kudidimia katika umaskini.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

24 Atoaye kwa ukarimu huzidi kutajirika; lakini bahili huzidi kudidimia katika umaskini.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

24 Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.

Tazama sura Nakili




Methali 11:24
19 Marejeleo ya Msalaba  

Azaria kuhani mkuu, wa nyumba ya Sadoki, akamjibu, akasema, Tangu watu walipoanza kuleta matoleo nyumbani kwa BWANA, tumekula na kushiba, na kusaza tele; kwa kuwa BWANA amewabariki watu wake; na kilichosalia ndiyo akiba hii kubwa.


Ametoa kwa ukarimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.


Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu; Apandaye haki ana thawabu ya hakika.


Haja ya mwenye haki ni kupata mema tu; Bali kutaraji kwake mtu mwovu huishia katika ghadhabu.


Nafsi ya mtu mkarimu itastawishwa; Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.


Kuna mtu anayejitajirisha, lakini hana kitu; Kuna anayejifanya kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.


Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.


Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiulegeze mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa, kama ni hii au hii, au kama zote zitafaa sawasawa.


Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamtosheki na vinywaji; mnajivika nguo lakini hampati joto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotobokatoboka.


Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.


Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.


Mpe kwa kweli, wala moyo wako usisikitike utakapompa; kwa kuwa atakubarikia BWANA, Mungu wako, kwa neno hili katika kazi yako yote, na katika kila utakalotia mkono wako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo