Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 14:22 - Swahili Revised Union Version

Je! Hawakosi wawazao mabaya? Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Anayepanga maovu kweli anakosea! Wanaopanga kutenda mema hufadhiliwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Anayepanga maovu kweli anakosea! Wanaopanga kutenda mema hufadhiliwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Anayepanga maovu kweli anakosea! Wanaopanga kutenda mema hufadhiliwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki? Bali wale wanaopanga kilicho chema hupata upendo na uaminifu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki? Bali wale wanaopanga kilicho chema hupata upendo na uaminifu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Je! Hawakosi wawazao mabaya? Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 14:22
19 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Na atukuzwe BWANA, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuacha rehema zake na kweli yake kwa bwana wangu. BWANA akaniongoza mimi nami njiani hata nyumba ya nduguze bwana wangu.


Lakini BWANA akamwambia Daudi baba yangu, Kwa kuwa ilikuwa moyoni mwako kujenga nyumba kwa jina langu, ulifanya vema kuwaza hivi moyoni mwako;


Njia zote za BWANA ni fadhili na kweli, Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.


Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.


Atakaa mbele za Mungu milele, Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.


Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.


Mwenye haki ni kiongozi wa mwenzake; Bali njia ya wasio haki huwakosesha.


Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.


Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.


Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo.


Mtu afikiriye kutenda maovu, Watu watamwita mtundu;


Usiwaze mabaya juu ya jirani yako, Ambaye anakaa karibu nawe na kujiona salama.


Rehema na kweli zisiachane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.


Mna upotovu moyoni mwake, hutunga uovu daima, Hupanda mbegu za magomvi.


Ole wao wakusudiao mambo maovu, na kutenda mabaya vitandani mwao! Kunapopambazuka asubuhi huyafanya, sababu wana uwezo mikononi mwao.


Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.


Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.


Wale wanaume wakamwambia, Tutautoa uhai wetu badala ya uhai wenu, ikiwa hamwitangazi habari ya shughuli yetu hii; kisha itakuwa, wakati BWANA atakapotupa nchi hii, tutakutendea kwa hisani na uaminifu.