Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 12:1 - Swahili Revised Union Version

Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Apendaye nidhamu hupenda maarifa, bali asiyependa kuonywa ni mjinga.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Apendaye nidhamu hupenda maarifa, bali asiyependa kuonywa ni mjinga.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Apendaye nidhamu hupenda maarifa, bali asiyependa kuonywa ni mjinga.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 12:1
21 Marejeleo ya Msalaba  

Unifahamishe njia ya maagizo yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.


Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.


Msiwe kama farasi wala nyumbu, Wasiokuwa na akili. Kwa matandiko ya lijamu na hatamu Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.


Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.


Mtu mjinga hayatambui hayo, Wala mpumbavu hayafahamu.


Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.


Ikiwa, mwenye haki atalipwa duniani; Je, mwovu na mkosaji hawatalipwa mara nyingi zaidi?


Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.


Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa.


Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.


Hakika nimekuwa kama mnyama, wala si mtu; Wala sina ufahamu wa mwanadamu;


Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.


Basi, wanangu, nisikilizeni sasa; Maana heri hao wazishikao amri zangu.


Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.


Ng'ombe amjua bwana wake, Na punda ajua kibanda cha bwana wake; Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.


naye kuhani ataangalia, ikiwa pana uvimbe mweupe katika ngozi yake, na mnywele zimegeuzwa kuwa nyeupe, tena ikiwa panafanyika kidonda katika ule uvimbe,


na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.