Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 18:1 - Swahili Revised Union Version

1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Anayetafuta yake tu hujitenga na wenzake; hukasirika akipewa shauri lolote jema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Anayetafuta yake tu hujitenga na wenzake; hukasirika akipewa shauri lolote jema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Anayetafuta yake tu hujitenga na wenzake; hukasirika akipewa shauri lolote jema.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.

Tazama sura Nakili




Methali 18:1
22 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana itajulikanaje kuwa nimepata neema mbele zako, mimi na watu wako? Siyo kwa sababu unakwenda pamoja nasi, hata mimi na watu wako tutengwe na watu wote walio juu ya uso wa nchi?


Moyo huujua uchungu wa nafsi yake, Wala mgeni haishiriki furaha yake.


Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji; Basi acheni ugomvi kabla haujafurika.


Mwenye udaku hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.


Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.


Mwanangu, mche BWANA, na mfalme; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;


Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake; Ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.


Mwanangu, yasiondoke haya machoni pako, Shika hekima kamili na busara.


Ushauri ni wangu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu.


Sikuketi katika mkutano wao wanaojifurahisha, wala sikufurahi, niliketi peke yangu kwa sababu ya mkono wako; kwa maana umenijaza ghadhabu.


na kusema na makuhani wa nyumba ya BWANA wa majeshi, na hao manabii, ya kwamba, Je! Yanipasa kulia katika mwezi wa tano, na kufunga, kama nilivyofanya miaka hii mingi iliyopita?


Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa.


Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile.


Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.


Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje, yote hufanywa kwa mifano,


Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;


Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.


na kila mnyama aliyepasuliwa ukwato, ukapasuka ukwato wake zikawa mbili, naye ni mnyama mwenye kucheua akatafuna tena, katika wanyama wote, ndiye mnyama mtakayemla.


Watu hao ndio waletao utengano, watu wa dunia hii tu, wasio na Roho.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo