Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 8:17 - Swahili Revised Union Version

17 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Nawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii hunipata.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Nawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii hunipata.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Nawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii hunipata.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii wataniona.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

17 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.

Tazama sura Nakili




Methali 8:17
22 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, naye akiwa bado mchanga, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi babaye; hata katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kusafisha Yuda na Yerusalemu kwa kuondoa mahali pa juu, na kwa kuondoa Maashera, na sanamu za kuchonga, na za kusubu.


Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.


Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.


Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;


Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, Na kupata kumjua Mungu.


Usimwache, naye atakusitiri; Umpende, naye atakulinda.


Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.


Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.


Kitambo kidogo tu nilipoachana nao, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena, Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu, Chumbani mwake aliyenizaa.


Sikusema kwa siri, katika mahali pa nchi ya giza; sikuwaambia wazao wa Yakobo; Nitafuteni bure; Mimi, BWANA, nasema ukweli; nanena mambo ya haki.


Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yuko karibu;


Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.


Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.


Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.


Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.


kwa maana Baba mwenyewe awapenda kwa kuwa ninyi mmenipenda mimi, na kusadiki ya kwamba mimi nilitoka kwa Baba.


Kwa maana kuna wakati ambapo malaika hushuka, akaingia katika lile bwawa, akayatibua maji. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona ugonjwa wote uliokuwa umempata.]


Katika siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.


Lakini mmoja wenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.


Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.


Kwa sababu hiyo, BWANA, Mungu wa Israeli, asema, Ni kweli, nilisema ya kuwa nyumba yako, na nyumba ya baba yako itakwenda mbele zangu milele; lakini sasa BWANA asema, Jambo hili na liwe mbali nami; kwa maana wao wanaoniheshimu nitawaheshimu, na wao wanaonidharau nitawadharau.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo