Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 16:1 - Swahili Revised Union Version

Wakamjia Mafarisayo na Masadukayo, wakamjaribu, wakamwomba awaoneshe ishara itokayo mbinguni.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mafarisayo na Masadukayo walimwendea Yesu, na kwa kumjaribu, wakamwomba awaoneshe ishara kutoka mbinguni.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mafarisayo na Masadukayo walimwendea Yesu, na kwa kumjaribu, wakamwomba awaoneshe ishara kutoka mbinguni.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mafarisayo na Masadukayo walimwendea Yesu, na kwa kumjaribu, wakamwomba awaoneshe ishara kutoka mbinguni.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Isa na kumjaribu kwa kumwomba awaoneshe ishara kutoka mbinguni.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Isa na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wakamjia Mafarisayo na Masadukayo, wakamjaribu, wakamwomba awaoneshe ishara itokayo mbinguni.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 16:1
33 Marejeleo ya Msalaba  

Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake.


Lakini wale Mafarisayo wakatoka wakafanya shauri juu yake jinsi ya kumwangamiza.


Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,


Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.


Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa sababu yoyote?


Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.


Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?


Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,


Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa;


Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato,


Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya Waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.


Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?


Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku wakimjaribu.


Tumpe, tusimpe? Naye, akijua unafiki wao, akawaambia, Mbona mmenijaribu? Nileteeni dinari niione.


Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza na kusema,


Na tazama, mwanasheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?


Wengine walimjaribu, wakimtaka afanye ishara itokayo mbinguni.


Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,


Kisha baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale wasemao ya kwamba hakuna ufufuo, wakamwuliza,


Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika ardhi.


Hata walipokuwa wakisema na watu wale, makuhani na walinzi wa hekalu na Masadukayo wakawatokea,


Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,


Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;