Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 19:1 - Swahili Revised Union Version

Afadhali maskini aendaye katika uadilifu wake, Kuliko mpotovu wa midomo aliye mpumbavu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Afadhali maskini aishiye kwa unyofu, kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Afadhali maskini aishiye kwa unyofu, kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Afadhali maskini aishiye kwa unyofu, kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Afadhali mtu maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama, kuliko mpumbavu ambaye midomo yake imepotoka.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Afadhali mtu maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama, kuliko mpumbavu ambaye midomo yake imepotoka.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Afadhali maskini aendaye katika uadilifu wake, Kuliko mpotovu wa midomo aliye mpumbavu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 19:1
16 Marejeleo ya Msalaba  

Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.


Mchana kutwa hufadhili na kukopesha, Na mzao wake hubarikiwa.


Mwenye haki ni kiongozi wa mwenzake; Bali njia ya wasio haki huwakosesha.


Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA; Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.


Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.


Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.


Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo.


Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.


Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotovu wa njia angawa ni tajiri.


Jiepushe na kinywa cha ujeuri, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.


Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong'ona uovu.


Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kuipoteza nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?


Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.


Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.