Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 26:11 - Swahili Revised Union Version

11 Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Lakini mimi ninaishi kwa unyofu; unihurumie na kunikomboa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Lakini mimi ninaishi kwa unyofu; unihurumie na kunikomboa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Lakini mimi ninaishi kwa unyofu; unihurumie na kunikomboa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.

Tazama sura Nakili




Zaburi 26:11
19 Marejeleo ya Msalaba  

Unikumbukie hayo, Ee Mungu wangu, wala usifute fadhili zangu nilizozitenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu, na kwa taratibu zake.


Kisha nikawaamuru Walawi wajitakase, nao waje kuyalinda malango, ili kuitakasa siku ya sabato. Unikumbukie hayo nayo, Ee Mungu wangu, ukaniachilie sawasawa na wingi wa rehema zako.


na kuleta kwa kuni na malimbuko, katika nyakati zilizoamriwa. Nikumbuke, Ee Mungu wangu, ili unitendee mema.


Lakini watawala wa kwanza walionitangulia, wakawalemea watu, wakawatwalia chakula na mvinyo, zaidi ya shekeli arubaini za fedha; tena hata watumishi wao nao wakawatawala watu; lakini mimi sikufanya hivyo, kwa kuwa nilimcha Mungu.


Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.


Nitakuwa na mwenendo usio na hatia; Utakuja kwangu lini? Nitakwenda kwa unyofu wa moyo Ndani ya nyumba yangu.


Ee BWANA, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini BWANA bila wasiwasi.


Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu, Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanipokea.


Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumlipa Mungu fidia kwa ajili ya maisha yake,


Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu unifidie.


akasema, Ee BWANA, kumbuka haya, nakusihi, kwamba nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia kwa uchungu.


Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiishi katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama.


Ninyi ni mashahidi, na Mungu pia, jinsi tulivyokaa kwenu ninyi mnaoamini, kwa utakatifu, na kwa haki, bila kulaumiwa;


ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wake mwenyewe walio na bidii katika matendo mema.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo