Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 19:2 - Swahili Revised Union Version

2 Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Haifai mtu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka hujikwaa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Haifai mtu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka hujikwaa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Haifai mtu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka hujikwaa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Sio vizuri kuwa na juhudi bila maarifa, wala kufanya haraka na kuikosa njia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Sio vizuri kuwa na juhudi bila maarifa, wala kufanya haraka na kuikosa njia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

Tazama sura Nakili




Methali 19:2
18 Marejeleo ya Msalaba  

Na mmoja wao akaenda nje kondeni ili kuchuma mboga, akaona mtangomwitu, akayachuma matangomwitu, hata nguo yake ikawa imejaa, akaja akayapasuapasua sufuriani; kwa maana hawakuyajua.


Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;


Maana miguu yao huenda mbio maovuni, Nao hufanya haraka ili kumwaga damu.


Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi; Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.


Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.


Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.


Usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania; Usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye, Mwenzako atakapokuwa amekuaibisha.


Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.


Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri; Wala haufikiri uhitaji utakaomjia.


Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.


Lakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akachunguza, akatunga mithali nyingi.


Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.


Matawi yake yatakapokauka yatavunjwa; wanawake watakuja na kuyachoma moto; kwa maana hawa si watu wenye akili; kwa sababu hiyo yeye aliyewaumba hatawahurumia, yeye aliyewafanya hatawasamehe.


kwa ajili ya hayo Bwana, MUNGU, asema hivi, Tazama, naweka jiwe katika Sayuni, liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani, msingi ulio imara; yeye aaminiye hatafanya haraka.


Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.


Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.


Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.


Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo