Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 20:7 - Swahili Revised Union Version

7 Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu; watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu; watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu; watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.

Tazama sura Nakili




Methali 20:7
18 Marejeleo ya Msalaba  

Agano langu nitalifanya imara kati yangu na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako.


Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.


Wazawa wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.


Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake,


Ee BWANA, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini BWANA bila wasiwasi.


Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.


Mchana kutwa hufadhili na kukopesha, Na mzao wake hubarikiwa.


Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.


Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA; Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.


Kumcha BWANA ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio.


Afadhali maskini aendaye katika uadilifu wake, Kuliko mpotovu wa midomo aliye mpumbavu.


Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung'utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za umwagaji wa damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.


nami nitawapa moyo mmoja na njia moja, wapate kunicha sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao;


Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiishi katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama.


Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.


Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo