Mistari ya Biblia

Matangazo


Vikundi Vidogo

119 Mistari ya Biblia kuhusu Kuombea Wengine

Rafiki, unajua njia bora ya kuonyesha upendo ni kumuomba Mungu kwa ajili ya wale wanaokuzunguka? Maombi yako yana nguvu kuliko maneno elfu moja utakayoyasema kwa uwezo wako mwenyewe.

Unapowaombea wengine, unaanza kuelewa shida wanazopitia, unahisi uchungu na mizigo yao, na roho yako inaguswa mpaka unalia mbele za Mungu kwa ajili yao. Kuna raha ya ajabu inayokujaa moyoni baada ya maombi hayo.

Unapowaombea wengine, unajiombea pia, jambo linalompendeza Mungu kwa sababu unawaza mema ya wengine badala ya yako mwenyewe. Biblia inatufundisha katika Waefeso 6:18 kuwaombea watakatifu wote kila wakati. Kuwa na tabia ya kusali ni muhimu sana ili tuweze kuwaombea wengine kila wakati.

Ukiwa huombelei wengine, unakosa kufanya mema kama Biblia inavyotuagiza. Ukimjali mtu, jambo bora unaloweza kufanya ni kumweka mbele za Mungu. Amua leo kuwa mwombezi, na amini kwamba kilio chako kinaweza kubadili mambo.

Unaweza kuokoa maisha, kurudisha ndoa, kuleta upatanisho katika familia, kupata msamaha na kuwafikia waliopotea kwa kumuomba rehema za Yesu tu. Ndiyo maana tunashauriana na kuombeana ili tupate kuponywa. Maombi ya mwenye haki yana nguvu na yana matokeo (Yakobo 5:16).


Zaburi 10:12

Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwaadhibu; usiwasahau wanaodhulumiwa.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 6:7

“Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 18:20

Kwa maana popote pale wanapokusanyika wawili au watatu kwa jina langu, mimi nipo hapo kati yao.”

Sura   |  Matoleo
Mathayo 6:6

Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.

Sura   |  Matoleo
1 Yohana 5:15

Yeye hutusikiliza kila tunapomwomba; na kwa vile tunajua kwamba yeye hutusikiliza kila tunapomwomba, twajua pia kwamba hutupatia yote tunayomwomba.

Sura   |  Matoleo
Yakobo 1:6

Lakini anapaswa kuomba kwa imani bila mashaka yoyote. Mtu aliye na mashaka ni kama mawimbi ya bahari ambayo husukumwa na kutupwatupwa na upepo.

Sura   |  Matoleo
Yohana 14:13

Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.

Sura   |  Matoleo
Matendo 1:14

Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.

Sura   |  Matoleo
Wafilipi 1:19

kwani najua kwamba kwa sala zenu na kwa msaada wa Roho wa Yesu Kristo, nitakombolewa.

Sura   |  Matoleo
Ezra 8:23

Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu atulinde, naye aliyasikia maombi yetu.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 5:44

Lakini mimi nawaambieni, wapendeni maadui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu nyinyi,

Sura   |  Matoleo
Marko 11:25

Mnaposimama kusali, msameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe nyinyi makosa yenu.” [

Sura   |  Matoleo
Matendo 12:5

Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.

Sura   |  Matoleo
Yeremia 33:3

“Niite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichika ambayo hujapata kuyajua.

Sura   |  Matoleo
Waroma 12:12

Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida, na kusali daima.

Sura   |  Matoleo
Yeremia 29:12

Hapo ndipo mtakaponiita na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Sura   |  Matoleo
Yohana 13:34

Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.

Sura   |  Matoleo
1 Wathesalonike 5:16-18

Furahini daima,

salini kila wakati

na kuwa na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.

Sura   |  Matoleo
Wafilipi 4:6-7

Msiwe na wasiwasi juu ya kitu chochote, ila kwa kila hali, mwombeni Mungu katika sala juu ya mahitaji yenu, kwa shukrani.

Nayo amani ya Mungu ipitayo akili zote za watu italinda salama mioyo na akili zenu katika kuungana na Kristo Yesu.

Sura   |  Matoleo
Wakolosai 4:2

Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.

Sura   |  Matoleo
1 Timotheo 2:1-2

Kwanza kabisa, nawasihi muombe dua, msali na kumshukuru Mungu kwa ajili ya watu wote,

bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.

Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.

Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.

Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.

Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.

Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.

kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.

Sura   |  Matoleo
Waroma 15:30

Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa Bwana wetu Yesu Kristo na kwa upendo uletwao na Roho, mniunge mkono kwa kuniombea kwa Mungu.

Sura   |  Matoleo
Wakolosai 1:9

Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu wakati tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa matakwa yake, pamoja na hekima yote na ujuzi wa kiroho.

Sura   |  Matoleo
1 Wathesalonike 5:25

Ndugu, tuombeeni na sisi pia.

Sura   |  Matoleo
Wafilipi 1:3-5

Namshukuru Mungu wangu kila ninapowakumbukeni;

Sasa mwaweza kushirikiana nami katika kupigana vita. Vita hivi ni vile mlivyoona nikipigana pale awali na ambavyo bado napigana sasa kama mnavyosikia.

na kila ninapowaombeeni nyote, nasali kwa furaha,

kwa sababu ya jinsi mlivyonisaidia katika kazi ya Injili tangu siku ile ya kwanza mpaka leo.

Sura   |  Matoleo
Wagalatia 6:2

Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 122:6

Uombeeni Yerusalemu amani: “Wote wakupendao na wafanikiwe!

Sura   |  Matoleo
Zaburi 55:17

Jioni, asubuhi na adhuhuri, nalalama na kulia, naye ataisikia sauti yangu.

Sura   |  Matoleo
1 Yohana 5:16

Mtu akimwona ndugu yake ametenda dhambi isiyompeleka kwenye kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, naye Mungu atampatia uhai. Nasema jambo hili kuhusu wale waliotenda dhambi ambazo si za kifo. Lakini ipo dhambi yenye kumpeleka mtu kwenye kifo, nami sisemi kwamba mnapaswa kumwomba Mungu kwa ajili ya hiyo.

Sura   |  Matoleo
1 Petro 4:8

Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 34:17

Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia, na kuwaokoa katika taabu zao zote.

Sura   |  Matoleo
Methali 15:29

Mwenyezi-Mungu yuko mbali na watu waovu, lakini yu karibu na watu wema kuwasikiliza.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 102:17

Ataikubali sala ya fukara; wala hatayakataa maombi yao.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 18:19-20

Tena nawaambieni, wawili miongoni mwenu wakikubaliana hapa duniani kuhusu jambo lolote la kuomba, Baba yangu wa mbinguni atawafanyia jambo hilo.

Yesu akamwita mtoto mmoja, akamsimamisha kati yao,

Kwa maana popote pale wanapokusanyika wawili au watatu kwa jina langu, mimi nipo hapo kati yao.”

Sura   |  Matoleo
Wakolosai 4:2-4

Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.

Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.

Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.

Sura   |  Matoleo
Waebrania 13:3

Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 126:5

Wanaopanda kwa machozi, watavuna kwa shangwe.

Sura   |  Matoleo
2 Wakorintho 1:11

nyinyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.

Sura   |  Matoleo
1 Samueli 12:23

Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Mwenyezi-Mungu; kufanya hivyo itakuwa kumkosea Mwenyezi-Mungu. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 141:2

Sala yangu uipokee kama ubani; niinuapo mikono yangu kwako unikubali kama tambiko ya jioni.

Sura   |  Matoleo
Luka 22:32

Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”

Sura   |  Matoleo
Zaburi 17:1-2

Ee Mwenyezi-Mungu usikie kisa changu cha haki, usikilize kilio changu, uitegee sikio sala yangu isiyo na hila.

Hao hawana huruma yoyote moyoni; wamejaa maneno ya kujigamba.

Wananifuatia na kunizunguka; wananivizia waniangushe chini.

Wako tayari kunirarua kama simba: Kama mwanasimba aviziavyo mawindo.

Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwakabili na kuwaporomosha. Kwa upanga uiokoe nafsi yangu kutoka kwa waovu.

Kwa mkono wako, ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe mikononi mwa watu hao, watu ambao riziki yao ni dunia hii tu. Uwajaze adhabu uliyowawekea, wapate ya kuwatosha na watoto wao, wawaachie hata na wajukuu zao.

Lakini mimi nitauona uso wako, kwani ni mwadilifu; niamkapo nitajaa furaha kwa kukuona.

Haki yangu na ije kutoka kwako, kwani wewe wajua jambo lililo la haki.

Sura   |  Matoleo
2 Mambo ya Nyakati 7:14

kama watu hao wangu wakijinyenyekesha, wakasali, wakanitafuta na kuacha njia zao mbaya, basi, mimi nitawasikiliza kutoka juu mbinguni; nitawasamehe dhambi yao na kuistawisha nchi yao.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 9:38

Basi mwombeni mwenye mavuno atume wafanyakazi wavune mavuno yake.”

Sura   |  Matoleo
Zaburi 68:20

Mungu wetu ni Mungu mwenye kutuokoa; Bwana Mungu pekee ndiye aokoaye katika kifo.

Sura   |  Matoleo
Waefeso 1:16-18

sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu,

ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.

Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,

Sura   |  Matoleo
Zaburi 86:6-7

Ee Mwenyezi-Mungu, uitegee sikio sala yangu; ukisikie kilio cha ombi langu.

Siku za taabu nakuita, maana wewe waniitikia.

Sura   |  Matoleo
2 Timotheo 1:3

Ninamshukuru Mungu ambaye ninamtumikia kwa dhamiri safi kama walivyofanya wazee wangu; namshukuru kila ninapokukumbuka katika sala zangu usiku na mchana.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 51:10-12

Uniumbie moyo safi, ee Mungu, uweke ndani yangu roho mpya na thabiti.

Usinitupe mbali nawe; usiniondolee roho yako takatifu.

Unifanye nifurahi tena kwa kuniokoa, utegemeze ndani yangu moyo wa utii.

Sura   |  Matoleo
Waroma 1:9

Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni

Sura   |  Matoleo
Zaburi 119:147-148

Naamka kabla ya pambazuko na kukuomba msaada; naweka tumaini langu katika maneno yako.

Nakaa macho usiku kucha, ili nitafakari juu ya maagizo yako.

Sura   |  Matoleo
Yakobo 1:5

Lakini kama mmoja wenu ametindikiwa hekima, basi, anapaswa kumwomba Mungu ambaye atampatia; kwani Mungu huwapa wote kwa wingi na kwa ukarimu.

Sura   |  Matoleo
Luka 18:1

Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 119:10

Najitahidi kukutii kwa moyo wote; usiniache nikiuke amri zako.

Sura   |  Matoleo
1 Wakorintho 12:26

Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.

Sura   |  Matoleo
Wakolosai 3:12

Nyinyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo, basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 30:8

Nilikulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu; naam niliomba dua kwako ee Mwenyezi-Mungu:

Sura   |  Matoleo
Isaya 53:12

Kwa hiyo, nitamweka katika cheo cha wakuu, atagawa nyara pamoja na wenye nguvu; kwa kuwa alijitolea mwenyewe kufa, akawekwa katika kundi moja na wakosefu, alizibeba dhambi za watu wengi, akawaombea msamaha hao wakosefu.”

Sura   |  Matoleo
Waebrania 10:24-25

Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.

Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, siku ile ya Bwana inakaribia.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 119:176

Natangatanga kama kondoo aliyepotea; uje kunitafuta mimi mtumishi wako, maana sikusahau amri zako.

Sura   |  Matoleo
1 Wathesalonike 3:10

Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 143:1

Usikie sala yangu, ee Mwenyezi-Mungu! Ulitegee sikio ombi langu maana wewe ni mwaminifu; unijibu kwa sababu ya uadilifu wako.

Sura   |  Matoleo
Wagalatia 4:19

Watoto wangu, kama vile mama mjamzito anavyotaabika wakati wa kujifungua, mimi nataabika tena kwa ajili yenu mpaka hapo hali yake Kristo itakapoundwa ndani yenu.

Sura   |  Matoleo
Methali 17:17

Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote, ndugu huzaliwa asaidie wakati wa taabu.

Sura   |  Matoleo
1 Yohana 3:22

na kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 8:4-5

mtu ni nini, ee Mungu, hata umfikirie, binadamu ni nini hata umjali?

Umemfanya awe karibu kama Mungu, umemvika fahari na heshima.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 26:41

Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho inataka lakini mwili ni dhaifu.”

Sura   |  Matoleo
Waroma 10:1

Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.

Sura   |  Matoleo
Matendo 16:25-26

Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.

Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 61:1-2

Ee Mungu, usikie kilio changu, usikilize sala yangu.

Ninakulilia kutoka miisho ya dunia, nikiwa nimevunjika moyo. Uniongoze juu kwenye mwamba mkubwa

Sura   |  Matoleo
Yakobo 5:14

Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 103:1-2

Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu; nafsi yangu yote ilisifu jina lake takatifu!

Yeye hatuadhibu kama tunavyostahili; hatulipizi kadiri ya uovu wetu.

Kama vile anga lilivyo juu mbali na dunia, ndivyo ulivyo mwingi wema wake kwa watu wanaomcha.

Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo azitengavyo dhambi zetu mbali nasi.

Kama vile baba amhurumiavyo mwanawe, ndivyo Mwenyezi-Mungu awahurumiavyo wote wamchao.

Mungu ajua mfumo wa nafsi zetu; ajua kwamba sisi ni mavumbi.

Walakini binadamu, maisha yake ni kama nyasi tu; huchanua kama ua shambani:

Upepo huvuma juu yake nalo latoweka; na mahali lilipokuwa hapaonekani tena.

Lakini fadhili za Mwenyezi-Mungu hudumu milele, kwa wale wote wanaomheshimu; na wema wake wadumu vizazi vyote,

kwa wote wanaozingatia agano lake, wanaokumbuka kutii amri zake.

Mwenyezi-Mungu ameweka kiti chake cha enzi mbinguni; yeye anatawala juu ya vitu vyote.

Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi-Mungu! Usisahau kamwe wema wake wote.

Sura   |  Matoleo
Wakolosai 1:3

Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.

Sura   |  Matoleo
Waroma 8:31-32

Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?

Mungu hakumhurumia hata Mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?

Sura   |  Matoleo
Zaburi 91:15

Akiniita, mimi nitamwitikia; akiwa taabuni nitakuwa naye; nitamwokoa na kumpa heshima.

Sura   |  Matoleo
2 Wakorintho 4:15

Yote haya ni kwa faida yenu, hata neema ya Mungu inapowafikia watu wengi zaidi na zaidi, shukrani nazo ziongezeke zaidi, kwa utukufu wa Mungu.

Sura   |  Matoleo
Methali 21:1

Moyo wa mfalme ni kama maji yanayotiririka; Mwenyezi-Mungu, huuongoza popote apendapo.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 25:7

Usikumbuke dhambi na makosa ya ujana wangu; unikumbuke kadiri ya fadhili zako, kwa ajili ya wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.

Sura   |  Matoleo
1 Wathesalonike 1:2

Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu nyinyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 88:13

Lakini mimi nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu; kila asubuhi nakuletea ombi langu.

Sura   |  Matoleo
Mathayo 7:7-8

“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni mlango, nanyi mtafunguliwa.

Maana, yeyote aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye mlango hufunguliwa.

Sura   |  Matoleo
1 Yohana 4:21

Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.

Sura   |  Matoleo
Waroma 8:38-39

Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: Wala kifo, wala uhai; wala malaika au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;

wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Sura   |  Matoleo
1 Petro 3:12

Maana Bwana huwatazama kwa wema waadilifu na kuzisikiliza sala zao. Lakini huwapa kisogo watu watendao maovu.”

Sura   |  Matoleo
Zaburi 130:1-2

Toka upeo wa unyonge wangu, nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.

Ee Bwana, sikia sauti yangu, uitegee sikio sauti ya ombi langu.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 119:43

Unijalie kusema ukweli wako daima, maana tumaini langu liko katika maagizo yako.

Sura   |  Matoleo
2 Wakorintho 10:4-5

Maana, silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu ya Mungu yenye kuharibu ngome zote. Tunaharibu hoja zote za uongo

na kubomoa kila kizuizi cha majivuno kilichowekwa kuipinga elimu ya Mungu; tunaziteka fikira zote na kuzifanya zimtii Kristo.

Sura   |  Matoleo
Wagalatia 3:26-27

Kwa njia ya imani, nyinyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu kwa kuungana na Kristo.

Nyinyi nyote mliobatizwa mkaungana na Kristo ni kama vile mmemvaa Kristo.

Sura   |  Matoleo
Wafilipi 2:4

Pasiwe na mtu anayetafuta faida yake mwenyewe tu bali faida ya mwenzake.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 18:6

Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Aliisikia sauti yangu hekaluni mwake; kilio changu kilimfikia masikioni mwake.

Sura   |  Matoleo
Waebrania 4:16

Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.

Sura   |  Matoleo
Waroma 12:15

Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wenye kulia.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 31:22

Nami niliogopa na kudhani kwamba ulikuwa umenitupa; kumbe, ulisikia kilio changu nilipokuita unisaidie.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 116:1-2

Nampenda Mwenyezi-Mungu, kwa maana anisikia, maana amesikia kilio cha ombi langu.

Nilikuwa na imani hata niliposema: “Mimi nimetaabika mno.”

Hata nilisema kwa hofu yangu: “Binadamu wote hawaaminiki!”

Nimrudishie nini Mwenyezi-Mungu, kwa ukarimu wote alionitendea?

Nitamtolea tambiko ya divai kwa kunikomboa, nitaomba kwa jina lake Mwenyezi-Mungu.

Nitamtimizia Mwenyezi-Mungu nadhiri zangu, mbele ya watu wake wote.

Kifo cha waaminifu wake Mwenyezi-Mungu si jambo dogo mbele yake.

Ee Mwenyezi-Mungu, mimi ni mtumishi wako; ni mtumishi wako, mtoto wa mjakazi wako; umenifungulia vifungo vyangu.

Nitakutolea tambiko za shukrani, na kukupa heshima zangu.

Nitakutimizia ahadi zangu, ee Mwenyezi-Mungu mbele ya watu wako wote,

waliokusanyika hekaluni mwako, katikati ya Yerusalemu. Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Yeye amenitegea sikio, hivyo nitamwomba muda wote niishio.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 119:28

Niko hoi kwa uchungu; unirudishie nguvu kama ulivyoahidi.

Sura   |  Matoleo
Methali 28:9

Anayekataa kuisikia sheria, huyo hata sala yake ni chukizo kwa Mungu.

Sura   |  Matoleo
Waefeso 6:19-20

Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Injili kwa uthabiti.

“Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,

Mimi ni balozi kwa ajili ya Injili hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 66:20

Asifiwe Mungu, maana hakuikataa sala yangu, wala kuondoa fadhili zake kwangu.

Sura   |  Matoleo
Wakolosai 4:12

Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu, anawasalimuni. Daima anawaombeeni nyinyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 139:23-24

Unichunguze, ee Mungu, unijue moyo wangu, unipime, uyajue mawazo yangu.

Uangalie kama mwenendo wangu ni mbaya, uniongoze katika njia ya milele.

Sura   |  Matoleo
Waroma 12:10

Pendaneni kindugu; kila mmoja amfikirie kwanza mwenzake kwa heshima.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 118:5

Katika taabu yangu nilimwomba Mwenyezi-Mungu, naye akanisikia na kuniweka huru.

Sura   |  Matoleo
1 Yohana 5:14

Na sisi tuko thabiti mbele ya Mungu kwani tuna hakika kwamba tukimwomba chochote kadiri ya matakwa yake, yeye hutusikiliza.

Sura   |  Matoleo
Waebrania 13:18

Mtuombee na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.

Sura   |  Matoleo
1 Petro 5:10

Lakini mkisha teseka muda mfupi, Mungu aliye asili ya neema yote na ambaye anawaiteni kuushiriki utukufu wake wa milele katika kuungana na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisheni na kuwapeni uthabiti, nguvu na msingi imara.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 54:2

Uisikie, ee Mungu, sala yangu; uyategee sikio maneno ya kinywa changu.

Sura   |  Matoleo
Zaburi 8:3-4

Nikiangalia mbingu, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizozisimika huko,

mtu ni nini, ee Mungu, hata umfikirie, binadamu ni nini hata umjali?

Sura   |  Matoleo
1 Mambo ya Nyakati 16:11

Mwendeeni Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu; mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.

Sura   |  Matoleo
Yobu 42:10

Baada ya Yobu kuwaombea rafiki zake, Mwenyezi-Mungu akamrudishia Yobu hali yake ya kwanza. Alimpa maradufu ya yote aliyokuwa nayo hapo awali.

Sura   |  Matoleo
Waefeso 6:18

Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.

Sura   |  Matoleo
1 Timotheo 2:1

Kwanza kabisa, nawasihi muombe dua, msali na kumshukuru Mungu kwa ajili ya watu wote,

Sura   |  Matoleo
Waroma 8:26-27

Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.

Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.

Sura   |  Matoleo
Yakobo 5:16

Basi, ungamanieni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.

Sura   |  Matoleo
Yohana 15:7

Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.

Sura   |  Matoleo
Wafilipi 4:6

Msiwe na wasiwasi juu ya kitu chochote, ila kwa kila hali, mwombeni Mungu katika sala juu ya mahitaji yenu, kwa shukrani.

Sura   |  Matoleo
Matendo 2:1

Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika mahali pamoja.

Sura   |  Matoleo

Maombi kwa Mungu

Ee Mungu wangu, Mwokozi wangu, Muumba wangu, nakusujudia. Wewe ni mkuu, mtakatifu, na wa thamani maishani mwangu. Rehema zako nyingi zimenilinda na kunipa nguvu. Ni neema yako tu inayonihifadhi na kunifanya niwe msikivu kwa mahitaji ya wengine. Siku ya leo nakuomba, Bwana, kwa jina la Yesu, kwa ajili ya maisha ya ndugu yangu (...). Mjaze nguvu katikati ya majaribu na mateso. Amani yako ipitayo akili zote imfunike ili aweze kutimiza kusudi lake kikamilifu. Weka mapenzi yako katika familia yake. Jitukuze Bwana, fanya kazi ya ajabu juu yake ili imani yake iimarike na asikate tamaa katika kazi yako. Mpe roho mpya iliyo imara ndani yake. Mjaze mafuta, ubariki kazi ya mikono yake. Fungua malango ya mbinguni ili apate fanaka katika kila jambo. Bwana, mfiche katika kivuli cha mbawa zako siku ya mabaya. Natangaza uponyaji wa kimwili na wa kiroho juu yake. Natangaza uhuru katika kila eneo la maisha yake. Natangaza kwamba adui hawezi kugusa roho yake, wala mali yake, wala kuumiza moyo wake, kwa sababu wewe Mungu ni ngao inayomzunguka, wewe ni utukufu wake, na wewe ndiye unayeinyanyua kichwa chake. Natangaza Baba mpendwa, kwamba maghala yake yatajaa tele na mashinikizo yake yatafurika divai. Naomba katika jina la Yesu, kwa sababu neno lako linasema: "Na ikiwa tunajua kwamba yeye hutusikia katika kila kitu tunachoomba, tunajua kwamba tuna maombi ambayo tumemwomba." Katika jina la Yesu, Amina.