Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 4:23 - Swahili Revised Union Version

Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana humo zatoka chemchemi za uhai.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana humo zatoka chemchemi za uhai.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana humo zatoka chemchemi za uhai.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 4:23
21 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Yehu hakuangalia, aende katika sheria ya BWANA, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote; hakutoka katika makosa ya Yeroboamu, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli.


Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; Na watu wakali hushika mali siku zote.


Yeye alindaye kinywa chake huilinda nafsi yake; Bali afunuaye midomo yake atapata uharibifu.


Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu; Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.


Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu; Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo.


Sikia, mwanangu, uwe na hekima, Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.


Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga; Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.


Mwanangu, yasiondoke haya machoni pako, Shika hekima kamili na busara.


Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.


Kuna balaa mbaya sana niliyoiona chini ya jua, nayo ni hii, mali alizoziweka mwenyewe kwa kujinyima;


Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?


Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.


Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wizi, ushuhuda wa uongo, na matukano;


Kesheni na kuomba, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.


Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.


Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako;


mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.