Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 19:29 - Swahili Revised Union Version

Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Adhabu iko tayari kwa wenye mzaha, mijeledi imetayarishwa kuchapa migongo ya wapumbavu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Adhabu iko tayari kwa wenye mzaha, mijeledi imetayarishwa kuchapa migongo ya wapumbavu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Adhabu iko tayari kwa wenye mzaha, mijeledi imetayarishwa kuchapa migongo ya wapumbavu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Adhabu zimeandaliwa kwa ajili ya wenye dhihaka na mapigo kwa ajili ya migongo ya wapumbavu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Adhabu zimeandaliwa kwa ajili ya wenye dhihaka na mapigo kwa ajili ya migongo ya wapumbavu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 19:29
17 Marejeleo ya Msalaba  

Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la BWANA. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arubaini na wawili miongoni mwao.


Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.


Enyi wajinga, hata lini mtapenda ujinga? Na wenye dharau kupenda dharau yao, Na wapumbavu kuchukia maarifa?


Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, Nitadhihaki hofu yenu ifikapo;


Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu; Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu.


Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu, Kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.


Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.


Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, Na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.


Hakika yake huwadharau wenye dharau, Bali huwapa wanyenyekevu neema.


Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng'ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;


Kama una hekima, una hekima kwa nafsi yako; Na kama una dharau, utaichukua peke yako.


Basi sasa msiwe watu wenye kudharau, vifungo vyenu msije vikakazwa; maana nimesikia kwa Bwana, BWANA wa majeshi, habari ya hukumu itakayotimizwa, nayo imekusudiwa, itakayoipata dunia yote pia.


Kwa maana mwenye kutisha ameangamizwa, naye mwenye dharau amekoma, nao wote watazamiao uovu wamekatiliwa mbali;


na iwe, ikimpasa kupigwa yule mwovu, alazwe chini na mwamuzi, na kupigwa mbele ya uso wake, kwa kadiri ya uovu wake, kwa kuhesabu.


Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humuonya Naye humpiga kila mwana amkubaliye.