Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 18:6 - Swahili Revised Union Version

6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Maneno ya mpumbavu huleta ugomvi; kila anachosema husababisha adhabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Maneno ya mpumbavu huleta ugomvi; kila anachosema husababisha adhabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Maneno ya mpumbavu huleta ugomvi; kila anachosema husababisha adhabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.

Tazama sura Nakili




Methali 18:6
14 Marejeleo ya Msalaba  

Ghadhabu ya mpumbavu hujulikana mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.


Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.


Mwenye hekima huhadhari, na kujitenga na uovu; Bali mpumbavu hupuuza yote, na hajali.


Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi, Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi.


Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji; Basi acheni ugomvi kabla haujafurika.


Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake, Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.


Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.


Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.


Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka; Naam, fitina na fedheha zitakoma.


Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.


Jiwe ni zito, na mchanga hulemea; Lakini ghadhabu ya mpumbavu ni nzito kuliko hivi vyote viwili.


Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo