Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 18:5 - Swahili Revised Union Version

5 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Si vizuri kumpendelea mtu mwovu, na kumnyima haki mtu mwadilifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Si vizuri kumpendelea mtu mwovu, na kumnyima haki mtu mwadilifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Si vizuri kumpendelea mtu mwovu, na kumnyima haki mtu mwadilifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

5 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.

Tazama sura Nakili




Methali 18:5
20 Marejeleo ya Msalaba  

Sembuse yeye huwajali nyuso za wakuu, Wala hawajali matajiri kuliko maskini? Kwani wote ni kazi ya mikono yake,


Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya?


Usiwafuate walio wengi kutenda uovu; wala usitie ushahidi wako katika neno lolote kwa kugeukia kando na kuandamana na mkutano ili kupotoa hukumu;


wala usimpendelee mtu mnyonge katika neno lake.


Usipotoe hukumu ya mtu maskini katika neno lake.


Yeye asemaye kwamba asiye haki ana haki; naye asemaye kwamba mwenye haki hana haki; Hao wote wawili ni chukizo kwa BWANA.


Tena kumwadhibu mwenye haki si vizuri; Wala si vyema kuwapiga wakuu kwa unyofu wao.


Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili. Kupendelea watu katika hukumu si kwema.


Kupendelea watu si kwema; Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.


Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.


wampao haki mwenye uovu, ili wapewe ijara, na kumwondolea mwenye haki haki yake!


Na hukumu imegeuka ikaenda nyuma, na haki inasimama mbali sana; maana kweli imeanguka katika njia kuu, na unyofu hauwezi kuingia.


Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu; bali utamhukumu jirani yako kwa haki.


Sikieni haya, tafadhali, enyi vichwa vya nyumba ya Yakobo, mnaoitawala nyumba ya Israeli, mnaochukia hukumu, na kuipotosha adili.


Mikono yao ni hodari kwa kutenda maovu; afisa na hakimu wanataka rushwa, mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.


Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, tunajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu.


Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza kesi wa wenye haki.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo