Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 1:1 - Swahili Revised Union Version

1 Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Heri mtu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki njia za wenye dhambi, wala kujumuika na wenye dharau;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Heri mtu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki njia za wenye dhambi, wala kujumuika na wenye dharau;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Heri mtu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki njia za wenye dhambi, wala kujumuika na wenye dharau;

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

Tazama sura Nakili




Zaburi 1:1
52 Marejeleo ya Msalaba  

Nafsi yangu, usiingie katika siri yao, Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao, Maana katika ghadhabu yao walimwua mtu, Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng'ombe;


Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.


Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.


Yeye naye akazifuata njia za nyumba ya Ahabu; kwa kuwa mamaye alikuwa mshauri wake katika kufanya maovu.


Je! Ni vema kwako wewe kuonea, Na kuidharau kazi ya mikono yako, Na kuiunga mkono mipango ya waovu?


Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mipango ya waovu na iwe mbali nami.


Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


Heri washikao hukumu, Na kutenda haki sikuzote.


Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake.


Enyi watenda mabaya, ondokeni kwangu, Niyashike maagizo ya Mungu wangu.


Heri watu wenye hali hiyo, Heri watu wenye BWANA kuwa Mungu wao.


Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, Na tumaini lake ni kwa BWANA, Mungu wake,


BWANA huwahifadhi wageni; Huwategemeza yatima na mjane; Bali njia ya wasio haki huiharibu.


Shikeni yaliyo bora, asije akafanya hasira Nanyi mkapotea njiani, Kwa kuwa hasira yake huwaka upesi; Heri wote wanaomkimbilia.


Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika kusanyiko kuu nitamhimidi BWANA.


Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumainia.


Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.


Unifiche mbali na njama za watenda mabaya, Mbali na mipango ya watu wafanyao maovu;


Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.


Ee BWANA wa majeshi, Heri mwanadamu anayekutumaini Wewe.


Mwanangu, usiende njiani pamoja nao; Uzuie mguu wako usiende katika mapito yao.


Enyi wajinga, hata lini mtapenda ujinga? Na wenye dharau kupenda dharau yao, Na wapumbavu kuchukia maarifa?


Ufahamu mwema huleta upendeleo; Bali njia ya muasi huangamiza.


Nenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.


Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.


Ili kukuokoa na njia ya uovu, Na watu wanenao yaliyopotoka;


Hakika yake huwadharau wenye dharau, Bali huwapa wanyenyekevu neema.


Njia ya waovu ni kama giza; Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho.


Kama una hekima, una hekima kwa nafsi yako; Na kama una dharau, utaichukua peke yako.


Sikuketi katika mkutano wao wanaojifurahisha, wala sikufurahi, niliketi peke yangu kwa sababu ya mkono wako; kwa maana umenijaza ghadhabu.


Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.


Kisha nikawaambia watoto wao jangwani, Msiende katika amri za baba zenu, wala msizishike hukumu zao, wala msijitie unajisi kwa vinyago vyao.


Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Baryona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.


Lakini yeye alisema, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.


(wala hakulikubali shauri na tendo lao), naye ni mtu wa Arimathaya, mji mmoja wa Wayahudi, tena anautazamia ufalme wa Mungu;


Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.


Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki.


ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu.


Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.


na kila mnyama aliyepasuliwa ukwato, ukapasuka ukwato wake zikawa mbili, naye ni mnyama mwenye kucheua akatafuna tena, katika wanyama wote, ndiye mnyama mtakayemla.


U heri, Israeli. Ni nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na BWANA! Ndiye ngao ya msaada wako, Na upanga wa utukufu wako; Na adui zako watajitiisha chini yako, Nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.


Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuishi katika uzinzi, tamaa, ulevi, na karamu za kula na kunywa vileo kupindukia, na ibada haramu ya sanamu;


Heri wazifuao nguo zao, ili wawe na haki ya kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo