Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 20:1 - Swahili Revised Union Version

1 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi; yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi; yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi; yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.

Tazama sura Nakili




Methali 20:1
21 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Daudi akamwalika, akala, akanywa mbele yake; naye akamlevya; hadi wakati wa jioni akatoka kwenda kulala kitandani mwake pamoja na watumishi wa bwana wake, lakini hakushuka nyumbani kwake.


Kisha Absalomu akawaamuru watumishi wake, akasema, Angalieni basi, moyo wake Amnoni utakapofurahiwa kwa mvinyo; nami nitakapowaambia, Mpigeni Amnoni, kisha mwueni, msiogope; si mimi niliyewaamuru? Iweni hodari, na wenye ujasiri.


Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.


Ee Lemueli, kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme; Wala haifai wakuu waseme, Kiko wapi kileo?


Lakini hawa nao wamekosa kwa divai, wamepotea kwa kileo; kuhani na nabii wamekosa kwa kileo, wamemezwa kwa divai, wamepotea kwa kileo; hukosa katika maono, hujikwaa katika hukumu.


Ole wao waamkao asubuhi na mapema, wapate kufuata kileo; wakishinda sana hadi usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao!


Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, na walio hodari wa kuchanganya vileo;


Husema, Njooni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi.


Uzinzi na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.


Sikukuu ya mfalme wetu, wakuu waliugua kwa ukali wa divai; alinyosha mkono wake pamoja na wenye mzaha.


Usinywe divai wala kileo chochote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu;


Naam, pamoja na hayo, divai ni mchumi mdanganyifu, mtu wa kiburi asiyekaa nyumbani mwake; huongeza tamaa yake kama kuzimu, naye huwa kama mauti, hawezi kushibishwa; bali hujikusanyia mataifa yote; hujiwekea kabila zote chungu chungu.


wala wezi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.


husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.


Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo