Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 15:2 - Swahili Revised Union Version

Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa, lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa, lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa, lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 15:2
14 Marejeleo ya Msalaba  

Moyo wangu umefurika kwa jambo jema, Mimi nasema niliyomfanyia mfalme; Ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi stadi.


Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye?


Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.


Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa; Bali mpumbavu hueneza upumbavu.


Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!


Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.


Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.


Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake; Huzidisha elimu ya midomo yake.


Upate kuilinda busara, Na midomo yako iyahifadhi maarifa.


Tena, upumbavu huongeza maneno; lakini mwanadamu hajui yatakayokuwako; nayo yatakayokuwa baada yake, ni nani awezaye kumweleza?


Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.


Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao.