Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 15:7 - Swahili Revised Union Version

7 Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa, lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa, lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa, lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.

Tazama sura Nakili




Methali 15:7
25 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako.


Kinywa chake mwenye haki hunena hekima, Na ulimi wake husema hukumu.


Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.


Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.


Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.


Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.


Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake; Huzidisha elimu ya midomo yake.


Upate kuilinda busara, Na midomo yako iyahifadhi maarifa.


Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kulia; Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto.


Bibi arusi, midomo yako yadondosha asali, Asali na maziwa viko chini ya ulimi wako; Na harufu ya mavazi yako Ni kama harufu ya Lebanoni.


Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba.


Enyi wazawa wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.


Akawaambia, Nendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.


Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.


Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha wengine vile vile.


Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfululizo wa maumbile, nao huwashwa moto na Jehanamu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo