Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 11:13 - Swahili Revised Union Version

Mwenye udaku hupitapita akifunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Apitapitaye akichongea hutoa siri, lakini anayeaminika rohoni huficha siri.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Apitapitaye akichongea hutoa siri, lakini anayeaminika rohoni huficha siri.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Apitapitaye akichongea hutoa siri, lakini anayeaminika rohoni huficha siri.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Masengenyo husaliti uaminifu, bali mtu mwaminifu hutunza siri.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwenye udaku hupitapita akifunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 11:13
14 Marejeleo ya Msalaba  

Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.


Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.


Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.


Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.


Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.


Mwenye udaku hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.


Ujitetee na mwenzako peke yake; Bali usiifunue siri ya mtu mwingine;


Ndipo wakuu wakamwendea Yeremia, wakamwuliza; naye akawaambia sawasawa na maneno aliyoamriwa na mfalme. Basi wakaacha kunena naye; maana neno lile halikujulikana.


Usiende huku na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usijifaidi kwa damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.


Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.


Wale wanaume wakamwambia, Tutautoa uhai wetu badala ya uhai wenu, ikiwa hamwitangazi habari ya shughuli yetu hii; kisha itakuwa, wakati BWANA atakapotupa nchi hii, tutakutendea kwa hisani na uaminifu.


Lakini wewe ukitangaza habari yetu hii, ndipo tutakuwa hatuna hatia, katika kiapo hiki ulichotuapisha.