Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 14:11 - Swahili Revised Union Version

Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwa maana yeyote anayejikweza atashushwa na anayejishusha, atakwezwa.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwa maana yeyote anayejikweza atashushwa na anayejishusha, atakwezwa.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kwa maana yeyote anayejikweza atashushwa na anayejishusha, atakwezwa.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 14:11
24 Marejeleo ya Msalaba  

Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa; Ila macho yako huwapinga wenye kiburi, uwadhili.


Basi mfalme akamwambia Hamani, Hima! Twaa mavazi na farasi kama ulivyosema, ukamfanyie vivyo hivyo Mordekai, Myahudi, aketiye mlangoni pa mfalme; lisipungue neno lolote katika yote uliyoyasema.


Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.


Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.


Maana Wewe wawaokoa watu wanaoonewa, Na macho ya kiburi utayadhili.


Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.


Amefanya nguvu kwa mkono wake; Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;


Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; Na wanyonge amewainua.


Akamwambia na yule aliyemwalika, Ufanyapo chakula cha mchana au cha jioni, usiwaite rafiki zako, wala ndugu zako, wala jamaa zako, wala jirani zako wenye mali; wao wasije wakakualika nawe ukapata malipo.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa;


Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.


Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;


Basi Samweli akasema, Ingawa ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa kuwa kichwa cha makabila ya Israeli? Naye BWANA akakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli.