Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yakobo 1:9 - Swahili Revised Union Version

9 Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Ndugu aliye maskini anapaswa kufurahi wakati Mungu anapomkweza,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Ndugu aliye maskini anapaswa kufurahi wakati Mungu anapomkweza,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Ndugu aliye maskini anapaswa kufurahi wakati Mungu anapomkweza,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Ndugu asiye na cheo kikubwa yampasa ajivunie hali hiyo maana ametukuzwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Ndugu asiye na cheo kikubwa yampasa ajivunie hali hiyo maana ametukuzwa.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

9 Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa;

Tazama sura Nakili




Yakobo 1:9
25 Marejeleo ya Msalaba  

Hakika binadamu ni ubatili, Na wenye cheo ni uongo, Katika mizani huinuka; Wote pamoja ni hafifu kuliko ubatili.


Amchekaye maskini humtukana Muumba wake; Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.


Afadhali maskini aendaye katika uadilifu wake, Kuliko mpotovu wa midomo aliye mpumbavu.


Wanyenyekevu nao wataongeza furaha yao katika BWANA, na maskini katika wanadamu watafurahi katika Mtakatifu wa Israeli.


Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; Na wanyonge amewainua.


Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


akawaambia, Yeyote atakayempokea mtoto huyu kwa jina langu anipokea mimi; na yeyote atakayenipokea mimi ampokea yeye aliyenituma. Kwa kuwa aliye mdogo miongoni mwenu nyote huyo ndiye mkubwa.


na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.


kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote.


Kwa maana maskini hawatakoma katika nchi milele; ndipo ninakuamuru na kukuambia, Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, maskini wako, katika nchi yako.


Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe, nduguzo mmojawapo, ndani ya malango yako mojawapo, katika nchi yako akupayo BWANA, Mungu wako, usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini;


Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia BWANA juu yako, ikawa ni dhambi kwako.


nakaza mwendo, niifikie tuzo la thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.


Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili.


Bali ninyi ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;


Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.


Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Humpandisha mhitaji kutoka jaani, Ili awaketishe pamoja na wakuu, Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu; Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA, Naye ameuweka ulimwengu juu yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo