Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 8:21 - Swahili Revised Union Version

Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mimi huwatajirisha wanaonipenda, huzijaza tele hazina zao wanipendao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mimi huwatajirisha wanaonipenda, huzijaza tele hazina zao wanipendao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mimi huwatajirisha wanaonipenda, huzijaza tele hazina zao wanipendao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

nawapa utajiri wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

nawapa utajiri wale wanipendao na kuzijaza hazina zao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 8:21
18 Marejeleo ya Msalaba  

Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali nyingi.


Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako kuna furaha tele; Na katika mkono wako wa kulia Mna mema ya milele.


Tutapata mali yote ya thamani, Tutazijaza nyumba zetu mateka.


Baraka ya BWANA hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo.


Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.


Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.


Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza.


Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.


Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.


Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.


Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.


na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.


Maana mliwaonea huruma wale waliokuwa katika vifungo, tena mkakubali kwa furaha kunyang'anywa mali zenu, mkijua kwamba nafsini mwenu mna mali iliyo njema zaidi, idumuyo.


tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.


Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.


Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Humpandisha mhitaji kutoka jaani, Ili awaketishe pamoja na wakuu, Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu; Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA, Naye ameuweka ulimwengu juu yake.