Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 21:20 - Swahili Revised Union Version

20 Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Nyumbani kwa mwenye busara mna hazina za thamani, lakini mpumbavu huponda mali yake yote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Nyumbani kwa mwenye busara mna hazina za thamani, lakini mpumbavu huponda mali yake yote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Nyumbani kwa mwenye busara mna hazina za thamani, lakini mpumbavu huponda mali yake yote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

20 Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

Tazama sura Nakili




Methali 21:20
20 Marejeleo ya Msalaba  

Amemeza mali, naye atayatapika tena; Mungu atayatoa tumboni mwake.


Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze; Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.


Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yadumu milele.


Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.


Baraka ya BWANA hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo.


Taji la wenye hekima ni mali zao; Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.


Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.


Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANA Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima.


Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.


Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, Na divai huyafurahisha maisha; Na fedha huleta jawabu la mambo yote.


Tena, kwa habari za kila mwanadamu, ambaye Mungu amempa mali na ukwasi, akamwezesha kula katika hizo, na kuipokea sehemu yake, na kuifurahia amali yake; hiyo ndiyo karama ya Mungu.


Hekima ni njema kama urithi; Naam, nayo ni bora kwao walionalo jua.


Lakini watu kumi walionekana miongoni mwao, waliomwambia Ishmaeli, Usituue; kwa maana tuna akiba zetu zilizofichwa shambani, za ngano, na shayiri, na mafuta, na asali. Basi, akawaacha, asiwaue watu hao pamoja na ndugu zao.


Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.


Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kubwa iliingia katika nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.


Tena, aliwaambia wanafunzi wake, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyekuwa na wakili wake; huyu alishitakiwa kwake kuwa anatapanya mali zake.


Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo