Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 3:3 - Swahili Revised Union Version

Rehema na kweli zisiachane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Utii na uaminifu visitengane nawe. Vifunge shingoni mwako; viandike moyoni mwako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Utii na uaminifu visitengane nawe. Vifunge shingoni mwako; viandike moyoni mwako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Utii na uaminifu visitengane nawe. Vifunge shingoni mwako; viandike moyoni mwako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Rehema na kweli zisiachane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 3:3
23 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa umekuja jana tu kwa nini nikusumbue leo, na kukuzungusha huku na huko pamoja nasi nami hapa ninaenda niwezapo kwenda? Rudi wewe, ukawarudishe na ndugu zako; rehema na kweli ziwe pamoja nawe.


Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.


Njia zote za BWANA ni fadhili na kweli, Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.


Fadhili na kweli zitakutana, Haki na amani zitakumbatiana.


Nayo itakuwa ishara kwako katika mkono wako, na kwa ukumbusho kati ya macho yako, ili kwamba sheria ya BWANA ipate kuwa kinywani mwako; kwani BWANA alikuondoa utoke Misri kwa mkono wenye uwezo.


BWANA akapita mbele yake, akatangaza, BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;


Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako.


Je! Hawakosi wawazao mabaya? Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.


Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.


Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme, Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili.


Yafunge hayo katika moyo wako daima; Jivike hayo shingoni mwako.


Zifunge katika vidole vyako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.


Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma, na kwa ncha ya almasi; imechorwa katika kibao cha moyo wao, na katika pembe za madhabahu zenu;


Lisikieni neno la BWANA, enyi wana wa Israeli; kwa maana BWANA ana shutuma nao wakaao katika nchi, kwa sababu hapana kweli, wala fadhili, wala kumjua Mungu katika nchi.


Sheria ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake; alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha uovu.


Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.


mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoiandaa, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.


kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;


Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako.


Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria zangu mioyoni mwao, Na katika fikira zao nitaziandika; ndipo anenapo,