Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 3:2 - Swahili Revised Union Version

2 Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Maana yatakupa wingi wa siku, maisha marefu na fanaka kwa wingi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Maana yatakupa wingi wa siku, maisha marefu na fanaka kwa wingi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Maana yatakupa wingi wa siku, maisha marefu na fanaka kwa wingi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.

Tazama sura Nakili




Methali 3:2
22 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe ukienda katika njia zangu, na kuyashika mausia yangu, na amri zangu, kama baba yako Daudi alivyokwenda, basi nitazifanya siku zako kuwa nyingi.


Utafika kaburini mwenye umri mtimilifu, Kama mganda wa ngano ulivyo wakati wake.


Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.


Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.


Alikuomba uhai, ukampa, Muda mrefu wa siku nyingi, milele na milele.


Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonesha wokovu wangu.


Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.


Kichwa chenye mvi ni taji la utukufu, Kama kikionekana katika njia ya haki.


Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu; Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.


Naye akanifundisha, akaniambia, Moyo wako uyahifadhi maneno yangu; Shika amri zangu ukaishi.


Maana, kwa msaada wangu siku zako zitazidishwa; Na miaka ya maisha yako itaongezwa.


Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima.


Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.


Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.


Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na muwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,


ili siku zenu zifanywe nyingi, na za vijana vyenu nao, juu ya nchi BWANA aliyowaapia baba zenu kuwa atawapa, kama zilivyo siku za mbingu juu ya nchi.


Tunzeni basi, mtende kama mlivyoamriwa na BWANA, Mungu wenu; msikengeuke kwa mkono wa kulia wala wa kushoto.


Maana, mazoezi ya viungo vya mwili yana manufaa kidogo, lakini utauwa una manufaa ya kila aina; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo