Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 20:3 - Swahili Revised Union Version

Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ni jambo la heshima kuepa ugomvi; wapumbavu ndio wanaogombana.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ni jambo la heshima kuepa ugomvi; wapumbavu ndio wanaogombana.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ni jambo la heshima kuepa ugomvi; wapumbavu ndio wanaogombana.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 20:3
17 Marejeleo ya Msalaba  

Kukawako ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abramu, na wachunga wanyama wa Lutu; na siku zile Wakanaani na Waperizi walikuwa wakikaa katika nchi.


Abramu akamwambia Lutu, Basi, usiwepo ugomvi, nakusihi, kati yangu na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wachungaji wako; maana sisi tu jamaa moja.


Naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatuma kwa Amazia mfalme wa Yuda, akisema, Mbaruti uliokuwako Lebanoni ulituma kwa mwerezi uliokuwako Lebanoni, kusema, Umwoze mwanangu binti yako; kukapita hayawani aliyekuwako Lebanoni, akaukanyaga ule mbaruti.


Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.


Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.


Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.


Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji; Basi acheni ugomvi kabla haujafurika.


Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.


Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.


Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.


Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake; Ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.


tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.


Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli.


Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?