Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 19:20 - Swahili Revised Union Version

Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa siku zijazo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa siku zijazo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa siku zijazo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Sikiliza mashauri na ukubali mafundisho, nawe mwishoni utakuwa na hekima.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Sikiliza mashauri na ukubali mafundisho, nawe mwishoni utakuwa na hekima.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 19:20
21 Marejeleo ya Msalaba  

Umwangalie sana mtu mkamilifu, Umtazame mtu mnyofu, Maana mwisho wake mtu huyo ni amani.


Basi, utufundishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.


Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako, Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote.


Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;


kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.


Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,


Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.


Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.


Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.


Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake, Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.


Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.


Ushauri ni wangu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu.


Sikieni mafundisho, mpate hekima, Wala msiikatae.


Uonyeke, Ee Yerusalemu, nafsi yangu, isije ikafarakana nawe; nisije nikakufanya ukiwa, nchi isiyokaliwa na watu.


Nilisema, Hakika utaniogopa, utakubali kurudiwa; ili yasikatiliwe mbali makao yake, sawasawa ya yote niliyoagiza katika habari zake; lakini waliondoka mapema na kuyaharibu matendo yao yote.


Ni nani awezaye kufanya idadi ya mavumbi ya Yakobo, Au kuhesabu robo ya Israeli? Na nife kifo chake mwenye haki, Na mwisho wangu uwe mfano wa mwisho wake.


Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu haya, Ili watafakari mwisho wao.


aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.