Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 6:8 - Swahili Revised Union Version

8 Uonyeke, Ee Yerusalemu, nafsi yangu, isije ikafarakana nawe; nisije nikakufanya ukiwa, nchi isiyokaliwa na watu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Hilo na liwe onyo kwako ee Yerusalemu, la sivyo nitakutupa kabisa kwa chuki; nikakufanya uwe jangwa, mahali pasipokaliwa na mtu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Hilo na liwe onyo kwako ee Yerusalemu, la sivyo nitakutupa kabisa kwa chuki; nikakufanya uwe jangwa, mahali pasipokaliwa na mtu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Hilo na liwe onyo kwako ee Yerusalemu, la sivyo nitakutupa kabisa kwa chuki; nikakufanya uwe jangwa, mahali pasipokaliwa na mtu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”

Tazama sura Nakili




Yeremia 6:8
23 Marejeleo ya Msalaba  

Na sasa, enyi wafalme, iweni na hekima, Enyi watawala wa dunia, mwaonywa.


Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.


Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;


Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.


Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.


lakini hawakusikiliza, wala hawakutega masikio yao, bali walifanya shingo zao kuwa ngumu, ili wasisikilize wala wasipokee mafundisho.


Wanasimba wamenguruma juu yake, wametoa sana sauti zao; Nao wameifanya nchi yake kuwa ukiwa; miji yake imeteketea, haina watu.


Hakika baada ya kukugeukia kwangu, nilitubu; na baada ya kufundishwa kwangu, nilijipiga pajani; nilitahayarika, naam, nilifadhaika, kwa sababu niliichukua aibu ya ujana wangu.


Tena wamenigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao; ingawa niliwafundisha, niliondoka mapema na kuwafundisha, lakini hawakusikiliza ili wapate mafundisho.


Ee Yerusalemu, jioshe moyo wako usiwe na uovu, upate kuokoka. Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini?


Kwa hiyo, Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, hasira yangu na ghadhabu yangu zitamwagwa juu ya mahali hapa, juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya miti ya mashamba, na juu ya mazao ya nchi; nayo itateketea, isizimike.


Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya BWANA, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali na vinywa vyao.


Ndipo katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu, nitaikomesha sauti ya kicheko na sauti ya furaha, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi; kwa maana nchi hiyo itakuwa ukiwa.


Nami nitafanya Yerusalemu kuwa magofu, Makao ya mbweha; Nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa, Isikaliwe na mtu awaye yote.


Basi alipoendelea na ukahaba wake waziwazi, na kufunua uchi wake; ndipo roho yangu ikafarakana naye, kama ilivyofarakana na dada yake.


Maana mama yao amezini; yeye aliyewachukua mimba ametenda mambo ya aibu; maana alisema, Nitafuatana na wapenzi wangu, wanipao chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na vileo vyangu.


Wajapolea watoto wao, mimi nitawanyang'anya watoto wao, asisalie hata mtu mmoja; naam, ole wao! Nitakapoondoka na kuwaacha.


Hapo ndipo nchi itakapozifurahia Sabato zake, wakati itakapokuwa hali ya ukiwa, nanyi mtakapokuwa katika nchi ya adui zenu; ndipo nchi itakapopumzika, na kuzifurahia Sabato zake.


Nilisema, Hakika utaniogopa, utakubali kurudiwa; ili yasikatiliwe mbali makao yake, sawasawa ya yote niliyoagiza katika habari zake; lakini waliondoka mapema na kuyaharibu matendo yao yote.


Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu haya, Ili watafakari mwisho wao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo