Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 15:32 - Swahili Revised Union Version

32 Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

32 Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe, bali anayekubali maonyo hupata busara.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

32 Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe, bali anayekubali maonyo hupata busara.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

32 Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe, bali anayekubali maonyo hupata busara.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

32 Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

32 Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

32 Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.

Tazama sura Nakili




Methali 15:32
27 Marejeleo ya Msalaba  

Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.


Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.


Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima; Bali yeye aachaye maonyo hukosa.


Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa; Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.


Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa; Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.


Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.


Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.


Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.


Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?


Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.


Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.


Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafla, wala hapati dawa.


Heri kusikia laumu ya wenye hekima, Kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu;


Mbona mnataka kupigwa, hata sasa, hata mkazidi kuasi? Kichwa chote ni kigonjwa, moyo wote umezimia.


Kuonekana kwa nyuso zao kwashuhudia juu yao, wafunua dhambi yao kama Sodoma, hawaifichi. Ole wa nafsi zao, kwa maana wamejilipa nafsi zao uovu.


Ee BWANA, macho yako je! Hayaangalii uaminifu? Umewapiga, lakini hawakuhuzunika; umewakomesha, lakini wamekataa kurudiwa wamefanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba wamekataa kurudi.


Mtu akiwa na mwana mkaidi, mshupavu, asiyetii sauti ya baba yake, wala sauti ya mama yake, nao wajapomwadhibu hawasikizi,


wawaambie wazee wa mji wake, Huyu mwana wetu ni mkaidi, mshupavu, hasikizi sauti yetu; ni mwasherati, tena ni mlevi.


mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.


Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.


Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo