Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 15:5 - Swahili Revised Union Version

Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mpumbavu hudharau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ana busara.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mpumbavu hudharau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ana busara.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mpumbavu hudharau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ana busara.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonesha busara.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 15:5
19 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Uwe hodari, mwenye moyo mkuu, ukatende hivyo; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu, Mungu wangu, yu pamoja nawe; yeye hatakupungukia wala kukuacha, hata itakapomalizika kazi yote ya huo utumishi wa nyumba ya BWANA.


Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele.


Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.


Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.


Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.


Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.


Mwana mwenye hekima husikiliza mausia ya babaye; Bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.


Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa; Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.


Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.


Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.


Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.


Kipuli cha dhahabu, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo.


Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.


Ushuhuda huo ni kweli. Kwa sababu hiyo uwakemee kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani;


Nena mambo hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.