Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 6:23 - Swahili Revised Union Version

23 Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 Maana amri hiyo ni taa, na sheria hiyo ni mwanga. Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 Maana amri hiyo ni taa, na sheria hiyo ni mwanga. Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 Maana amri hiyo ni taa, na sheria hiyo ni mwanga. Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 Kwa maana amri hii ni taa, mafundisho haya ni mwanga, na maonyo ya nidhamu ni njia ya uzima,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

23 Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.

Tazama sura Nakili




Methali 6:23
22 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu.


Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.


Kufafanuliwa kwa maneno yako kunatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.


Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.


Maagizo ya BWANA ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya BWANA ni safi, Huyatia macho nuru.


Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima; Bali yeye aachaye maonyo hukosa.


Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.


Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.


Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.


Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu anayeshikamana naye.


Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.


Naye akanifundisha, akaniambia, Moyo wako uyahifadhi maneno yangu; Shika amri zangu ukaishi.


Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo, Na moyo wangu ukadharau kukemewa;


Nami nimeona lililo na uchungu kupita mauti; yaani, mwanamke ambaye moyo wake ni mitego na tanzi, na mikono yake ni kama vifungo; yeye ampendezaye Mungu atamponyoka, bali mwenye dhambi atanaswa na yeye.


Heri kusikia laumu ya wenye hekima, Kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu;


Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi kulingana na neno hili, bila shaka kwa hao hakuna asubuhi.


Nawe waambie watu hawa, BWANA asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.


Nikawapa amri zangu, na kuwaonesha hukumu zangu, ambazo mwanadamu ataishi kwazo, kama akizitenda.


Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, au ulipizwe uovu kwa ajili yake


Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa iangazayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu.


Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo