Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 26:49 - Swahili Revised Union Version

Mara akamwendea Yesu, akasema, Salamu, Rabi, akambusu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mara Yuda akamjia Isa na kumsalimu, “Salamu, Mwalimu!” Akambusu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mara Yuda akamjia Isa na kumsalimu, “Salamu, Mwalimu!” Akambusu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mara akamwendea Yesu, akasema, Salamu, Rabi, akambusu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 26:49
15 Marejeleo ya Msalaba  

Isaka, baba yake, akamwambia, Njoo karibu sasa, ukanibusu, mwanangu.


Naye Yoabu akamwambia Amasa, Amani kwako, ndugu yangu. Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kulia ili ambusu.


Majeraha utiwazo na rafiki ni ya kweli; Bali busu la adui ni udanganyifu.


na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.


Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.


Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.


Na yule mwenye kumsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni.


wakaanza kumsalimu, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!


Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.


Wakawa wakimwendea, wakisema, Salamu! Mfalme wa Wayahudi! Wakampiga makofi.


Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.


Wasalimieni ndugu wote kwa busu takatifu.


Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! BWANA hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa BWANA, na kuwaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa BWANA amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake.