Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 22:7 - Swahili Revised Union Version

Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Tajiri humtawala maskini; mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Tajiri humtawala maskini; mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Tajiri humtawala maskini; mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Matajiri huwatawala maskini naye akopaye ni mtumwa wa akopeshaye.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Matajiri huwatawala maskini naye akopaye ni mtumwa wa akopeshaye.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 22:7
16 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha, akasema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha BWANA; na aliyemdai amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa.


Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.


Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali.


Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara.


Usimnyang'anye maskini, kwa kuwa ni maskini; Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;


Na itakuwa kama ilivyo hali ya watu, ndivyo itakavyokuwa hali ya kuhani; kama ilivyo hali ya mtumwa, ndivyo itakavyokuwa hali ya bwana wake; kama ilivyo hali ya mjakazi, ndivyo itakavyokuwa hali ya bibi yake; kama ilivyo hali yake anunuaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake auzaye; kama ilivyo hali yake akopeshaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake akopaye; kama ilivyo hali yake atwaaye faida, ndivyo itakavyokuwa hali yake ampaye faida.


Haya ndiyo asemayo BWANA; Kwa makosa matatu ya Israeli, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu;


Lisikieni neno hili, enyi ng'ombe wa Bashani, mnaokaa juu ya mlima wa Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao, Haya! Leteni, tunywe.


Lisikieni hili, ninyi mnaopenda kuwameza wahitaji, na kuwakomesha maskini wa nchi,


tupate kuwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu; na kuziuza takataka za ngano.


Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, ikalipwe ile deni.


Bali ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri hawawaonei ninyi na kuwavuta mbele ya viti vya hukumu?


Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige mayowe kwa sababu ya mateso yenu yanayowajia.


Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliokosa kuwalipa kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.