Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 19:3 - Swahili Revised Union Version

Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya BWANA.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake, huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake, huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake, huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Upumbavu wa mtu mwenyewe huharibu maisha yake hata hivyo moyo wake humkasirikia Mwenyezi Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Upumbavu wa mtu mwenyewe huharibu maisha yake hata hivyo moyo wake humkasirikia bwana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya BWANA.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 19:3
21 Marejeleo ya Msalaba  

Hata alipokuwa katika kusema nao, tazama, yule aliyetumwa akamshukia; naye akasema, Angalia, mabaya haya yatoka kwa BWANA; kwani mimi kumngojea BWANA tena?


Hata ukageuza roho yako kinyume cha Mungu, Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.


Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya, Usiwahusudu wafanyao ubatili.


Utulie mbele za BWANA, Nawe umngojee kwa subira; Usihangaike juu ya afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu apangaye maovu.


Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.


Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya BWANA, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa bila chakula, na kuwanyima kinywaji wenye kiu.


Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?


Lakini ninyi mwasema, Njia ya Bwana si sawa. Sikilizeni sasa, Enyi nyumba ya Israeli; Je! Njia yangu siyo iliyo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa?


Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya BWANA, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana BWANA angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele.


Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama uovu na kuabudu vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.