Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Maombolezo 3:39 - Swahili Revised Union Version

39 Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

39 Kwa nini mtu anung'unike, ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

39 Kwa nini mtu anung'unike, ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

39 Kwa nini mtu anung'unike, ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

39 Je, mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

39 Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

39 Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?

Tazama sura Nakili




Maombolezo 3:39
27 Marejeleo ya Msalaba  

Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, Nina nini mimi nawe? Uende kwa manabii wa babayo, na manabii wa mamayo. Mfalme wa Israeli akamwambia, La, sivyo; kwa kuwa BWANA amewakutanisha hawa wafalme watatu, awaue mkononi mwa Moabu.


Lakini Elisha alikuwa akikaa nyumbani mwake, na wazee wakikaa pamoja naye; na mfalme akamtuma mtu wa mbele yake; lakini hata kabla ya kufika kwake yule aliyetumwa, akawaambia wazee, Je! Mwaona jinsi huyu mwana wa mwuaji alivyotuma aniondolee kichwa changu? Angalieni, huyo aliyetumwa akifika, fungeni mlango, mkamzuie mlangoni; je! Sauti ya miguu ya bwana wake haiko nyuma yake?


Hata alipokuwa katika kusema nao, tazama, yule aliyetumwa akamshukia; naye akasema, Angalia, mabaya haya yatoka kwa BWANA; kwani mimi kumngojea BWANA tena?


Na baada ya hayo yote yaliyotupata kwa sababu ya matendo yetu mabaya, na kwa sababu ya hatia yetu iliyo kuu, ikiwa wewe Mungu wetu hukutuadhibu kama tulivyostahili kwa maovu yetu, maana umetupa mabaki;


Tena akuoneshe hizo siri za hekima, Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake! Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.


Hata ukageuza roho yako kinyume cha Mungu, Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.


Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.


Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya BWANA.


Wana wako wamezimia, Wamelala penye pembe za njia kuu zote Kama kulungu wavuni; Wamejaa hasira ya BWANA, Lawama ya Mungu wako.


Ole wangu, kwa sababu ya jeraha langu! Pigo langu laumia; lakini nilisema, Kweli, ni huzuni yangu mimi, nami sina budi kuivumilia.


Mbona unalilia maumivu yako? Maumivu yako hayaponyeki; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka, nimekutenda haya.


Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.


mimi nami nimewaendea kinyume, na kuwatia katika nchi ya adui zao; lakini hapo, kama mioyo yao isiyokuwa tohara ikinyenyekea, nao wakubali adhabu ya uovu wao;


Nchi nayo itaachwa na wao, nayo itazifurahia Sabato zake, itakapokuwa ukiwa pasipokuwa na wao; nao wataikubali adhabu ya uovu wao; kwa sababu wameyakataa maagizo yangu, na roho zao zimezichukia amri zangu.


Nitaivumilia ghadhabu ya BWANA, kwa kuwa nimemwasi; hata atakaponitetea shutuma yangu, na kunifanyia hukumu; atanileta nje kwenye nuru, nami nitaiona haki yake.


Musa akamwambia BWANA, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu?


Lakini siku ya pili yake mkutano wote wa wana wa Israeli wakamnung'unikia Musa, na Haruni, wakasema, Ninyi mmewaua watu wa BWANA.


Kisha wana wa Israeli wakanena na Musa, na kumwambia, Angalia, sisi tunakufa, tunaangamia, sote tunaangamia.


Wanadamu wakaunguzwa na joto kali, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo