Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 15:24 - Swahili Revised Union Version

Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai, ili aepe kuingia chini kuzimu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai, ili aepe kuingia chini kuzimu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai, ili aepe kuingia chini kuzimu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima kumwepusha asiende chini kaburini.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima kumwepusha asiende chini kaburini.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 15:24
15 Marejeleo ya Msalaba  

Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele.


Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako kuna furaha tele; Na katika mkono wako wa kulia Mna mema ya milele.


Maana nyumba yake inaelekea mauti, Na mapito yake yanakwenda kwenye wafu.


Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.


Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi kung'aa hata mchana mkamilifu.


Miguu yake inateremkia mauti; Hatua zake zinashikamana na kuzimu;


Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.


Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.


Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia; Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.


Nawe waambie watu hawa, BWANA asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.


Bali mlango ni mwembamba, na njia imebana iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.


Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.


Maana, moto umewashwa kwa hasira yangu, Unateketea hata chini ya kuzimu, Unakula dunia pamoja na mazao yake, Unaunguza misingi ya milima.


Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;