Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 7:28 - Swahili Revised Union Version

Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati wa watu ukashangazwa na mafundisho yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati wa watu ukashangazwa na mafundisho yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati wa watu ukashangazwa na mafundisho yake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa alipomaliza kusema maneno haya, umati wa watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 7:28
18 Marejeleo ya Msalaba  

Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.


Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.


Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika katika eneo la Yudea, ng'ambo ya Yordani.


Na makutano waliposikia, walishangaa kwa mafunzo yake.


Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,


mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.


kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka, wala si kama waandishi wao.


Wakashangaa mno kwa mafundisho yake; kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka, wala si kama waandishi.


Wakuu wa makuhani na waandishi wakapata habari wakatafuta jinsi ya kumwangamiza; maana walimwogopa, kwa sababu mkutano wote walishangazwa na mafundisho yake.


Na ilipokuwa sabato, alianza kufundisha katika sinagogi; wengi waliposikia wakashangaa, wakisema, Huyu ameyapata wapi haya? Na, Ni hekima gani hii aliyopewa huyu? Na, Ni nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake?


wasione la kutenda, kwa kuwa watu wote walikuwa wakiandamana naye, wakimsikiliza.


Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.


Wakamshuhudia wote, wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu?


wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa kuwa neno lake lilikuwa na uwezo.


Alipokwisha kuyamaliza maneno yake yote masikioni mwa watu, aliingia Kapernaumu.


Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma?


Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu yeyote kama huyu anavyonena.