Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 3:16 - Swahili Revised Union Version

BWANA akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu asema: “Wanawake wa Siyoni wana kiburi; wanatembea wameinua shingo juu, wakipepesa macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, na miguuni njuga zinalia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu asema: “Wanawake wa Siyoni wana kiburi; wanatembea wameinua shingo juu, wakipepesa macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, na miguuni njuga zinalia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu asema: “Wanawake wa Siyoni wana kiburi; wanatembea wameinua shingo juu, wakipepesa macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, na miguuni njuga zinalia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwenyezi Mungu asema, “Wanawake wa Sayuni wana kiburi, wanatembea na shingo ndefu, wakikonyeza kwa macho yao, wanatembea kwa hatua za madaha, wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

bwana asema, “Wanawake wa Sayuni wana kiburi, wanatembea na shingo ndefu, wakikonyeza kwa macho yao, wanatembea kwa hatua za madaha, wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 3:16
16 Marejeleo ya Msalaba  

Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.


Mwenye kiburi na moyo wa majivuno, Taa yake ni dhambi.


Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana.


Tokeni, enyi binti za Sayuni, Mtazameni Mfalme Sulemani, Amevaa taji alilovikwa na mamaye, Siku ya posa yake, Siku ya furaha ya moyo wake.


Na binti Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kipenu katika shamba la matango, kama mji uliohusuriwa.


Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.


Kwa maana, tazama, Bwana, BWANA wa majeshi, awaondolea Yerusalemu na Yuda egemeo na tegemeo; tegemeo lote la chakula na tegemeo lote la maji;


Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na BWANA ataifunua aibu yao.


Siku hiyo BWANA atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;


Nami nitawapa watoto kuwamiliki, na watoto wachanga kuwatawala.


hapo Bwana atakapokuwa ameuosha uchafu wa hao binti za Sayuni na kuisafisha damu ya Yerusalemu kati yake, kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza.


Siku ile hutaaibishwa kwa matendo yako yote uliyoniasi; maana hapo nitawaondoa watu wako wanaojigamba na kujivuna, wasiwe kati yako, wala hutatakabari tena katika mlima wangu mtakatifu.


Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwanapunda, mtoto wa punda.


Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.