Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 16:18 - Swahili Revised Union Version

18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Kiburi hutangulia maangamizi; majivuno hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Kiburi hutangulia maangamizi; majivuno hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Kiburi hutangulia maangamizi; majivuno hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Kiburi hutangulia maangamizi, roho ya majivuno hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Kiburi hutangulia maangamizi, roho ya majivuno hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.

Tazama sura Nakili




Methali 16:18
27 Marejeleo ya Msalaba  

Hata Hamani alipoona ya kwamba Mordekai hamwinamii wala kumsujudia, alighadhibika sana.


Basi Hamani akaingia. Mfalme akamwambia, Afanyiwe nini yule ambaye mfalme apenda kumheshimu? Hamani akasema moyoni mwake, Ni nani ambaye mfalme apenda kumheshimu kuliko mimi?


Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.


Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.


Apendaye ugomvi hupenda dhambi; Auinuaye sana mlango wake hutafuta uharibifu.


Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.


Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.


Kumcha BWANA ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.


Ikawa alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza, wanawe, wakampiga kwa upanga; wakakimbilia nchi ya Ararati; naye Esar-hadoni, mwanawe, akatawala baada yake.


Kuhusu kuogofya kwako, Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Ushikaye kilele cha milima; Ujapofanya kiota chako juu sana kama tai, Nitakushusha kutoka huko; asema BWANA.


Na mwenye kiburi atajikwaa, na kuanguka, wala hapana atakayemwinua; nami nitawasha moto katika miji yake, nao utawala wote wamzungukao pande zote.


Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama.


Nayo nchi ya Misri itakuwa ukiwa na jangwa; nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA; kwa sababu amesema, Mto huu ni wangu, nami nimeufanya.


Atakapokwisha kuchukua lile jeshi, moyo wake utatukuzwa; naye atawaangusha makumi ya maelfu; lakini hataongezewa nguvu.


Na wewe, mwanawe, Ee Belshaza, hukujinyenyekeza moyo wako, ijapokuwa ulijua hayo yote.


Ndipo kile kiganja cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa.


Ndipo akaanza kulaani na kuapa akisema, Simjui mtu huyu. Na mara jogoo akawika.


akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya kushika mahali pa nyuma.


Vema. Yalikatwa kwa kutoamini kwao, na wewe wasimama kwa imani yako. Usijivune, bali uogope.


Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.


Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuusikiza ujumbe aliotumiwa na Yeftha.


Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo