Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hosea 5:6 - Swahili Revised Union Version

Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe wamtafute BWANA; lakini hawatamwona; amejitenga nao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe, kumtafuta Mwenyezi-Mungu; lakini hawataweza kumpata, kwa sababu amejitenga nao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe, kumtafuta Mwenyezi-Mungu; lakini hawataweza kumpata, kwa sababu amejitenga nao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe, kumtafuta Mwenyezi-Mungu; lakini hawataweza kumpata, kwa sababu amejitenga nao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wanapoenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe kumtafuta Mwenyezi Mungu, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe kumtafuta bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe wamtafute BWANA; lakini hawatamwona; amejitenga nao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hosea 5:6
23 Marejeleo ya Msalaba  

Musa akamjibu, Tutakwenda na vijana wetu na wazee wetu, na wana wetu, na binti zetu, tutakwenda na kondoo zetu na ng'ombe zetu; kwa kuwa inatupasa kumfanyia BWANA sikukuu.


Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.


Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.


Sadaka ya wasio haki ni chukizo; Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!


Nilimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; (Nimezimia nafsi yangu aliponena), Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie.


Yeye achinjaye ng'ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao.


Basi, BWANA asema hivi, Tazama, nitaleta mabaya juu yao, ambayo hawataweza kuyakimbia; nao watanililia, lakini sitawasikiliza.


Basi, usiwaombee watu hawa, wala usipaze sauti yako, wala kuwaombea dua watu hawa; maana sitawasikia wakati watakaponililia kwa ajili ya taabu yao.


Wafungapo, mimi sitasikia kilio chao; na watoapo sadaka za kuteketezwa na sadaka ya unga, sitazitakabali; bali nitawaangamiza kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni.


Msitumainie maneno ya uongo, mkisema, Hekalu la BWANA, Hekalu la BWANA, Hekalu la BWANA ndiyo haya.


Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite.


Kwa sababu hiyo mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitawaonea huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza.


Akaniambia, Mwanadamu, je! Unayaona wanayoyafanya, yaani, haya machukizo makubwa wanayoyafanya nyumba ya Israeli hapa, ili niende zangu mbali na patakatifu pangu? Lakini utaona tena machukizo makubwa mengine.


Kwa habari za dhabihu za matoleo yangu, hutoa dhabihu ya nyama na kuila; lakini BWANA hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao, na kuwapatiliza dhambi zao; watarudi kwenda Misri.


Nao watatangatanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huku na huko, kulitafuta neno la BWANA, wasilione.


Ndipo watakapomwomba BWANA, asiwaitikie; naam, atawaficha uso wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.


Laiti angekuwapo kwenu mtu mmoja wa kuifunga milango; msije mkawasha moto bure madhabahuni pangu! Sina furaha kwenu, asema BWANA wa majeshi, wala sitakubali dhabihu yoyote mikononi mwenu.


Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba.


Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja.