Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mika 3:4 - Swahili Revised Union Version

4 Ndipo watakapomwomba BWANA, asiwaitikie; naam, atawaficha uso wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Wakati unakuja ambapo mtamlilia Mwenyezi-Mungu, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mmetenda mambo maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Wakati unakuja ambapo mtamlilia Mwenyezi-Mungu, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mmetenda mambo maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Wakati unakuja ambapo mtamlilia Mwenyezi-Mungu, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mmetenda mambo maovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Kisha watamlilia Mwenyezi Mungu, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Kisha watamlilia bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Ndipo watakapomwomba BWANA, asiwaitikie; naam, atawaficha uso wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.

Tazama sura Nakili




Mika 3:4
26 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Mungu atakisikia kilio chake, Taabu zitakapomfikia?


Hakika Mungu hatasikia ubatili, Wala Mwenyezi hatauangalia.


Walipiga yowe, lakini hakuna wa kuokoa, Walimwita BWANA lakini hakuwajibu,


Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.


Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, Hata sala yake ni chukizo.


Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.


Ole wake mtu mbaya; shari itakuwa kwake, kwa maana atapewa malipo ya mikono yake.


Basi, BWANA asema hivi, Tazama, nitaleta mabaya juu yao, ambayo hawataweza kuyakimbia; nao watanililia, lakini sitawasikiliza.


Wafungapo, mimi sitasikia kilio chao; na watoapo sadaka za kuteketezwa na sadaka ya unga, sitazitakabali; bali nitawaangamiza kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni.


Wanakuja kupigana na Wakaldayo, lakini ni kuzijaza kwa mizoga ya watu, niliowaua katika hasira yangu na ghadhabu yangu, ambao kwa ajili ya uovu wao wote nimeuficha mji huu uso wangu.


Manabii wanatabiri uongo, na makuhani wanatawala kwa msaada wa hao; na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo. Nanyi mtafanya nini mwisho wake?


Kwa sababu hiyo mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitawaonea huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza.


Na hao waonaji wataaibika, na wenye kubashiri watafadhaika; naam, hao wote watajifunika midomo yao; kwa maana; hapana jawabu la Mungu.


Hata hivyo nchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya hao wakaao ndani yake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.


Ikawa kama wakati nilipowaita, wasitake kunisikiliza; basi, nao wataniita, wala sitasikiliza, asema BWANA wa majeshi.


Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?


Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;


Tunajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo.


Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.


Nanyi mtalia siku ile kwa sababu ya mfalme wenu mliyejichagulia; BWANA asiwajibu siku ile.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo