Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Samueli 2:9 - Swahili Revised Union Version

Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake; Bali waovu watanyamazishwa gizani, Maana kwa nguvu hakuna atakayeshinda;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Maisha ya waaminifu wake huyalinda, lakini maisha ya waovu huyakatilia mbali gizani. Maana, binadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Maisha ya waaminifu wake huyalinda, lakini maisha ya waovu huyakatilia mbali gizani. Maana, binadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Maisha ya waaminifu wake huyalinda, lakini maisha ya waovu huyakatilia mbali gizani. Maana, binadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake; Bali waovu watanyamazishwa gizani, Maana kwa nguvu hakuna atakayeshinda;

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Samueli 2:9
41 Marejeleo ya Msalaba  

Atakimbizwa kutoka mwangani hata gizani, Na kufukuzwa atoke duniani.


Wafiche mavumbini pamoja, Wafunge nyuso zao mahali palipositirika.


Basi hivi huyo maskini ana matumaini, Na uovu hufumba kinywa chake.


Nawe utajua ya kwamba hema yako ni salama; Na zizi lako utalikagua, wala usikose kitu.


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


Akawatoa wakiwa na fedha na dhahabu, Katika makabila yao asiwepo mwenye kujikwaa.


Hatauacha mguu wako usogezwe; Akulindaye hatasinzia;


BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli katika mkono wako wa kulia.


BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.


BWANA huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza.


Ee BWANA, nisiaibishwe, maana nimekuita; Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni.


Kwa kuwa BWANA hupenda haki, Wala hawaachi watauwa wake. Wao hulindwa milele, Bali mzawa wa wasio haki ataharibiwa.


Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee BWANA, fadhili zako zilinitegemeza.


Enyi mmpendao BWANA, uchukieni uovu; Huwalinda nafsi zao watauwa wake, Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki.


Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake.


Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.


Kwa kuwa BWANA atakuwa tumaini lako, Naye atakulinda mguu wako usinaswe.


Siku zake zote hula gizani, mwenye fadhaa nyingi, mwenye ugonjwa na uchungu.


Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.


Mimi, BWANA, nililinda, Nitalitia maji kila dakika, Asije mtu akaliharibu; Usiku na mchana nitalilinda.


Kaa kimya, ingia gizani, Ee binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena Malkia wa falme.


Mbona tunakaa kimya? Jikusanyeni, tukaingie ndani ya miji yenye maboma, tukanyamaze humo kwa maana BWANA, Mungu wetu, ametunyamazisha, naye ametupa maji yenye uchungu tunywe, kwa sababu tumemwasi BWANA.


BWANA asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake;


Lakini kwa gharika ifurikayo atapakomesha kabisa mahali pake, na kuwafuatia adui zake hata gizani.


Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,


Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la BWANA kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema BWANA wa majeshi.


BWANA akubariki, na kukulinda;


bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


Basi twajua ya kuwa mambo yote inenayo torati huyanena kwa hao walio chini ya torati, ili kila kinywa kifumbwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu;


Hakika awapenda hayo makabila ya watu; Watakatifu wake wote wamo mkononi mwako; Nao waliketi miguuni pako; Watapokea kila mmoja katika maneno yako.


Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani ili mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho.


Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa.


Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, kwa hao walioitwa, waliopendwa katika Mungu Baba, na kuhifadhiwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.


Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, niliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.


Basi sasa, bwana wangu, aishivyo BWANA, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa BWANA amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.