Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 2:5 - Swahili Revised Union Version

Mamaye akawaambia watumishi, Lolote atakalowaambia, fanyeni.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mama yake akawaambia wale watumishi, “Fanyeni lolote atakalowaambia.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mamaye akawaambia watumishi, Lolote atakalowaambia, fanyeni.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 2:5
12 Marejeleo ya Msalaba  

Na nchi yote ya Misri ilipoona njaa, watu walimlilia Farao awape chakula. Farao akawaambia Wamisri wote, Nendeni kwa Yusufu; atakavyowaambia, fanyeni.


Ndivyo alivyofanya Nuhu, sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.


Nikafanya vile vile kama nilivyoamriwa; nilitoa vyombo vyangu wakati wa mchana kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa, na wakati wa jioni nikautoboa ukuta kwa mkono wangu; nikavitoa gizani, nikavichukua begani, mbele ya macho yao.


Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye.


Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.


Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.


Kwa imani Abrahamu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako.


naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;


Asile kitu chochote kitokacho katika mzabibu, wala asinywe divai, wala mvinyo, wala asile kitu chochote kilicho najisi; hayo yote niliyomwamuru na ayatunze.


Basi akashuka mpaka ugani; akafanya yote kama vile mkwewe alivyomwagiza.