Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 15:14 - Swahili Revised Union Version

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Nyinyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Nyinyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Nyinyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.

Tazama sura Nakili




Yohana 15:14
19 Marejeleo ya Msalaba  

na Azaria mwana wa Nathani alikuwa afisa mkuu tawala; na Zabudi mwana wa Nathani alikuwa kuhani, rafiki yake mfalme.


Maana alishikamana na BWANA, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake BWANA alizomwamuru Musa.


Si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako hata milele?


Musa na Haruni wakafanya vivyo hivyo; kama BWANA alivyowaambia, ndivyo walivyofanya.


Ajifanyiaye marafiki wengi ni kwa maangamizi yake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.


Naingia bustanini mwangu, dada yangu, bibi arusi, Nachuma manemane yangu na rihani, Nala sega la asali na asali yangu, Nanywa divai yangu na maziwa. Kaleni, rafiki zangu, kanyweni, Naam, nyweni sana, wapendwa wangu.


Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Abrahamu, rafiki yangu;


nao wakaingia, wakaimiliki; lakini hawakuitii sauti yako, wala hawakuenda katika sheria yako; hawakutenda neno lolote katika haya uliyowaagiza wayatende; basi, kwa sababu hii umeleta juu yao mabaya haya yote;


Nikafanya vile vile kama nilivyoamriwa; nilitoa vyombo vyangu wakati wa mchana kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa, na wakati wa jioni nikautoboa ukuta kwa mkono wangu; nikavitoa gizani, nikavichukua begani, mbele ya macho yao.


Kwa maana yeyote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye kaka yangu, na dada yangu na mama yangu.


Nami nawaambia ninyi rafiki zangu, msiwaogope hao wauuao mwili, kisha baada ya hayo hawana wawezalo kutenda zaidi.


Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.


Mkinipenda, mtazishika amri zangu.


Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.


Mlisikia ya kwamba mimi niliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.


Mamaye akawaambia watumishi, Lolote atakalowaambia, fanyeni.


Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Abrahamu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu.


Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.


Basi akashuka mpaka ugani; akafanya yote kama vile mkwewe alivyomwagiza.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo