Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Matendo 9:6 - Swahili Revised Union Version

6 Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Sasa inuka uingie mjini, nawe utaambiwa unachopaswa kufanya.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 “Sasa inuka uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

6 Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.

Tazama sura Nakili




Matendo 9:6
33 Marejeleo ya Msalaba  

Ni nani amchaye BWANA? Atamfundisha katika njia anayoichagua.


Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;


Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia.


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Akaniambia, Mwanadamu, simama kwa miguu yako, nami nitasema nawe.


Na mkono wa BWANA ulikuwako juu yangu huko; akaniambia, Ondoka, nenda bondeni; nami nitasema nawe huko.


Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.


Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.


Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi?


Wakasema, Kornelio jemadari, mtu mwenye haki, mchaji wa Mungu, aliye na sifa njema kwa taifa lote la Wayahudi, alionywa na malaika mtakatifu kutuma watu kwako, uende nyumbani kwake, ili asikilize kile utakachosema.


Basi, tuma watu kwenda Yafa, ukamwite Simoni aitwaye Petro, anakaa katika nyumba ya Simoni, mtengenezaji wa ngozi, karibu na pwani; naye akija atasema nawe.


Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda.


Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?


Nikasema, Nifanye nini, Bwana? Bwana akaniambia, Simama, uingie Dameski, na huko utaambiwa habari za mambo yote yaliyoamriwa uyafanye.


Lakini inuka, usimame kwa miguu yako, maana nimekutokea kwa sababu hii, nikuweke wewe uwe mtumishi na shahidi wa mambo haya uliyoyaona, na wa mambo ambayo katika hayo nitajidhihirisha kwako;


Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayemtesa.


Na Isaya anao ujasiri mwingi, asema, Nilipatikana nao wasionitafuta, Nilidhihirika kwao wasioniulizia.


Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.


Lakini sheria iliingia ili kosa lile liwe kubwa sana; na dhambi ilipozidi, neema ilikuwa nyingi zaidi;


Nami nilikuwa hai hapo kwanza bila sheria; ila ilipokuja ile amri, dhambi ilihuika, nami nikafa.


Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.


Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.


Umwalike Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonesha utakayotenda; nawe utampaka mafuta yule nitakayemtaja kwako.


Basi alipowaona hao majeshi ya Wafilisti, huyo Sauli akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo