Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 9:8 - Swahili Revised Union Version

Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia; Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia; mwonye mwenye hekima naye atakupenda.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia; mwonye mwenye hekima naye atakupenda.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia; mwonye mwenye hekima naye atakupenda.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Usimkemee mwenye dhihaka, la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia; Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 9:8
23 Marejeleo ya Msalaba  

Wakamwambia mfalme wakasema, Tazama, Nathani, nabii. Naye alipoingia ndani mbele ya mfalme, akamsujudia kifudifudi.


Naye mfalme Daudi akasema, Niitie Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada. Nao wakaingia ndani mbele ya mfalme.


Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Yupo mtu mmoja, ambaye tungeweza kumwuliza BWANA kwa yeye, yaani Mikaya mwana wa Imla; lakini namchukia; kwa sababu hanibashirii mema, ila mabaya. Yehoshafati akasema, La! Mfalme asiseme hivi.


Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.


mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.


Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.


Mwana mwenye hekima husikiliza mausia ya babaye; Bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.


Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa; Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.


Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima.


Mpige mwenye mzaha, na mjinga atapata busara; Mwonye mwenye ufahamu, naye atatambua maarifa.


Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.


Usiseme masikioni mwa mpumbavu; Maana atadharau hekima ya maneno yako.


Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali; Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.


Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafla, wala hapati dawa.


Lakini watu wakanyamaza kimya; wala hawakumjibu hata neno moja; maana ilikuwa amri ya mfalme, kwamba, Msimjibu neno.


Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, au ulipizwe uovu kwa ajili yake


Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.


Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.