Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 28:4 - Swahili Revised Union Version

Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Watu wanaovunja sheria huwasifu waovu, lakini wanaoishika sheria hupingana nao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Watu wanaovunja sheria huwasifu waovu, lakini wanaoishika sheria hupingana nao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Watu wanaovunja sheria huwasifu waovu, lakini wanaoishika sheria hupingana nao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wale wanaoacha sheria huwasifu waovu, bali wale wanaotii sheria huwapinga.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 28:4
31 Marejeleo ya Msalaba  

Naye akajibu, Si mimi niliyewataabisha Israeli; bali ni wewe, na nyumba ya baba yako, kwa kuwa mmeziacha amri za BWANA; nawe umewafuata mabaali.


Naye Eliya akawakaribia watu wote, akanena, Mtasitasita katikati ya mawazo mawili hata lini? BWANA akiwa ndiye Mungu, mfuateni; bali ikiwa Baali ni Mungu, haya! Mfuateni yeye. Wale watu hawakumjibu neno.


Siku hizo niliona katika Yuda watu wengine waliosindika zabibu ili kupata mvinyo siku ya sabato, na wengine waliochukua miganda, na kuwapakia punda zao; tena na mvinyo, na zabibu, na tini, na namna zote za mizigo, waliyoileta Yerusalemu, siku ya sabato; nami nikashuhudia juu yao siku ile waliyouza vyakula.


Na mwana mmoja wa Yoyada, mwana wa Eliashibu, kuhani mkuu, alikuwa mkwewe Sanbalati, Mhoroni, basi nikamfukuza kwangu.


Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.


Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai, Na watu watakusifu ukijitendea mema,


Jambo la ajabu, la kuchukiza, limetokea katika nchi hii!


Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.


Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Ndipo akakubali.


Na alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazawa wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?


Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya mungu, si sauti ya mwanadamu.


Basi baada ya Paulo na Barnaba kushindana na watu hawa na kuhojiana nao sana, ndugu wakaamuru kwamba Paulo na Barnaba na wengine miongoni mwao wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee ili kuzungumza juu ya suala hilo.


Lakini wengine walikaidi, wakakataa kuamini, wakiitukana ile Njia mbele ya mkutano; basi, akaondoka akawaacha, akawatenga wanafunzi, akahojiana na watu kila siku katika darasa la mtu mmoja, jina lake Tirano.


ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.


Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;


ingawa tuliteswa na kutukanwa, katika Filipi kama mjuavyo, tulithubutu katika Mungu kuinena Injili ya Mungu kwenu, kwa kuishindania sana.


Hao ni wa dunia; kwa hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia.


Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, niliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.