Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 10:3 - Swahili Revised Union Version

3 Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Mwovu hujisifia tamaa zake mbaya, mtu wa tamaa hulaani na kumkataa Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Mwovu hujisifia tamaa zake mbaya, mtu wa tamaa hulaani na kumkataa Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Mwovu hujisifia tamaa zake mbaya, mtu wa tamaa hulaani na kumkataa Mwenyezi-Mungu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Hujivunia tamaa za moyo wake; humbariki mlafi na kumtukana Mwenyezi Mungu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Hujivunia tamaa za moyo wake; humbariki mlafi na kumtukana bwana.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.

Tazama sura Nakili




Zaburi 10:3
40 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha ujihesabie jeshi, kama jeshi ulilopoteza, farasi kwa farasi na gari kwa gari; nasi tutapigana nao katika nchi tambarare, na bila shaka tutawashinda. Akaisikiliza sauti yao, akafanya kama hivyo.


Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;


Nao wananifumbulia vinywa vyao, Husema, Ewe! Ewe! Jicho letu limeona.


Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai, Na watu watakusifu ukijitendea mema,


Ambao wanazitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao;


Utawaharibu wasemao uongo; BWANA humchukia mwuaji na mwenye hila


Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.


Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?


Adui akasema, Nitafuata, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.


Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao.


Mambo hayo yote nimeyaona mimi katika siku za ubatili wangu, yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake, yuko na mtu mwovu azidishaye maisha yake katika udhalimu wake.


Ni nani uliyemshutumu na kumtukana? Umeinua sauti yako juu ya nani, na kuinua macho yako juu? Juu ya Mtakatifu wa Israeli.


Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake niliona hasira, nikampiga; nilificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe.


Bali macho yako na moyo wako hauna utakalo ila kutamani, na kumwaga damu isiyo na hatia, na kudhulumu, na kutenda jeuri.


Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia.


Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kiota chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu!


Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.


Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.


Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,


ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.


wala wezi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.


Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, (ndiye mwabudu sanamu), aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.


ikawa asikiapo maneno ya laana hii, ajibarikie mtu huyo moyoni mwake, na kusema, Nitakuwa katika amani, nijapotembea katika upotoe wa moyo wangu kwa kuangamiza mbichi na kavu;


BWANA akaona, akawachukia, Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake.


Basi, viueni viungo vyenu vilivyo vya kidunia, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;


Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;


Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya.


Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.


Naye akamwambia mama yake, Hizo fedha elfu na mia moja ulizoibiwa, na kuweka laana kwa ajili yake na kusema masikioni mwangu, tazama, ninazo mimi hizo fedha; ni mimi niliyezitwaa. Mama yake akasema, Mwanangu na abarikiwe na BWANA.


Naye Sauli akasema, Na mbarikiwe ninyi na BWANA; kwa sababu mmenihurumia.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo